.

.

.

.

Friday, April 03, 2015

CHEF ISSA KIPANDE AFUNGUA MGAHAWA WA KISASA NCHINI SWEDEN





IMG_1647
Mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande akizungumza machache na wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kutoa risala ya ufunguzi.
IMG_1656
IMG_1926
Meza kuu wakifuatilia historia ya Chef Issa Kapande (hayupo pichani) wakati akizungumza na wageni waalikwa.
IMG_1980
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akisoma risala mara baada ya kuzindua mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden unaomilikiwa na mtanzania Chef Issa Kapande.
IMG_1951
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago akitambulishwa kwa wageni waalikwa.
IMG_1650
Baadhi wageni waalikwa wakisikiliza historia ya Chef Issa Kapande kabla ya mgeni rasmi kusoma risala ya ufunguzi.
IMG_1669
Ukumbi mzima ulionekana kuvutiwa na historia ya maisha na mafanikio ya Mtanzania Chef Issa Kapande (hayupo pichani).
IMG_1685
Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund (kushoto) akimkabidhi zawadi ya picha Chef Issa Kapande ambapo alimuomba aitafutie nafasi ndani ya mgahawa wake kama kumbukumbu.
IMG_1699
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu (kushoto) na mwenyeji wake Meya na mwenyekiti wa Trollhattan, Paul Akerlund pamoja na Makamu mwenyekiti wa kamati ya elimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Trollhattans Stad, Fahime Nordborg (kulia) wakiongoza wageni waalikwa 300 kushiriki chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mmiliki wa mgahawa huo Chef, Issa Kapande.
IMG_1700
IMG_1708
Chef Issa Kapande akikata nyama ya Mbuzi kwa ajili ya mgeni rasmi, Mh, Balozi Dora Msechu.
IMG_1712
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu akifurahi jambo na Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya Shamy Tours and Travel Agent Zanzibar, Khamis Mwinjuma Simba (kushoto).
IMG_1715
Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund akijisevia minofu ya nyama ya Mbuzi wakati wa uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_1742
Wageni wakiendelea kupakua chakula.
IMG_1769
IMG_1775
IMG_1798
IMG_1816
IMG_1821
IMG_1756
Mwenyekiti wa awali wa Chama cha Watanzania waishio Sweden (TANRIKS), Tengo Kilumanga (kulia) na mkewe wakishiriki chakula cha jioni kwenye mgahawa wa Mtanzania mwezao.
IMG_1824
Katibu wa Chama cha Watanzania Sweden (TANRIKS), Mathias Pembe (kushoto) pamoja na Mhasibu wa chama hicho, Bw. Emmanuel Ntundu ni miongoni kati ya wageni waalikwa 300 waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_1835
IMG_1838
Katibu wa Chama cha Watanzania Sweden (TANRIKS), Mathias Pembe (kulia), Mhasibu wa chama hicho, Bw. Emmanuel Ntundu (kushoto) pamoja na mtoto wa Mwenyekiti wa chama hicho, Grace Saulli wakijichana msosi uliondaliwa na Chef Issa Kapande.
IMG_1866
Wageni waalikwa wakiendelea kupiga msosi uliofurahiwa na wengi ambao utakuwa unapatikana kwa chakula cha mchana kwa kipindi cha mwezi mmoja na hapo baadae itakuwa mpaka chakula cha usiku ndani ya mgahawa wa "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food).
IMG_1869
Mh. Balozi Dora Msechu na mwenyeji wake Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund.
IMG_2028
Mgeni rasmi Mh. Balozi Dora Msechu kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
IMG_2080
Mgeni rasmi Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mh. Dora Msechu (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa chama cha Watanzania waishio Sweden (TANRIKS), Daniel Saulli (kushoto), Mhasibu wa chama hicho, Emmanuel Ntundu (kulia), Katibu wa chama hicho, Mathias Pembe (wa pili kulia) pamoja na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago.
IMG_2265
Mgeni rasmi Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Mh. Dora Msechu (wa pili kulia) na Mtanzania ambaye ni mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden, Chef Issa Kapande katika picha ya pamoja kikundi cha burudani.........
IMG_2216
Mtanzania ambaye ni mmiliki wa mgahawa unaotoa huduma za chakula cha kitanzania unaofahamika kama "Lunch by Chef Issa" (The house of Tanzanian food) uliopo katika mji wa Trollhattan, Sweden, Chef Issa Kapande katika picha ya kumbukumbu na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago.
IMG_2237
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania, Tagie Daisy Mwakawago, Chef Issa Kapande katika picha ya pamoja na timu yake kwenye mgahawa huo.
IMG_2041
Mdau Abraham Juma Ndwatta wa Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden akiwa na Grace Saulli kwenye hafla ya uzinduzi wa mgahawa huo.
IMG_2074
Wadau wakiendelea kupiga picha na Mh. Balozi Dora Msechu.
IMG_2125
Mh. Balozi Dora Msechu akisakata rhumba kwenye uzinduzi huo.
IMG_2093
Chef Issa Kapande akicheza muziki na wageni waalikwa.
IMG_2119


No comments:

Post a Comment