MAREHEMU WILLIAM VEDASTUS MUGURUSI (1943 – 2013)
Familia ya Marehemu, Bwana William Vedastus Mugurusi
wa Kijitonyama Dar es Salaam, inapenda kutoa shukurani zake za dhati kwa wale
wote walioshiriki nao katika kumuuguza na hatimaye kifo cha mume, baba, kaka na
babu yao mpendwa kilichotokea siku ya Jumanne tarehe 16.04.2013 katika hospitali ya AMI Wellness Center na kuzikwa Ijumaa
tarehe 19.04.2013 katika makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam.
Shukurani za pekee ziwaendee madaktari wote na wauguzi
wa hospitali za Apollo,(India) Aga Khan na Ami Wellness Center ambao walijaribu
kwa kadri ya uwezo wao kuokoa maisha ya mpendwa wetu; Uongozi na timu nzima ya
Globe Accountancy Service (GAS) kwa ushirikianao wao wa hali na mali; Mapadri
na wahudumu wote wa Kanisa Katoliki kwa huduma za kiroho; AAR, FHI360, ndugu,
jamaa, marafiki, wanajumuiya ya Mt. Damiano Mfia Dini, na majirani wote.
Kutokana na ukweli kwamba siyo rahisi kumshukuru kilammoja kwa jina, tunapenda kuwahakikishia kwamba tunathamini ushiriki wa kila mmoja kwa njia ya pekee, ushiriki ambao umeendelea kutupa faraja wakati wa kipindi hiki kigumu.
Tunawasihi tafadhali kila mmoja apokee shukrani zetu za dhati katika uzito ule
ule.
Kutakuwa na misa ya shukrani tarehe 25 May 2013, saa 4 asubuhi nyumbani kwa marehemu William Vedastus Mugurusi, Kijitonyama.
WOTE MNAKARIBISHWA.
Thursday, May 23, 2013
MISS KURASINI 2013 YAPAMBA MOTO
Baadhi ya wanyange wanaowania taji la Redd’s Miss Kurasini 2013 wakiwa wakijifua kwa kucheza wimbo wa ufunguzi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa Equator Grill wakijifua kwa shindano lao linalotaraji kufanyika katika ukumbi huo leo.
Washiriki wa Redd’s Miss Kurasini 2013, wakimsikiliza mwalimu wao Kudra Lupatu wakati warembo hao wakiendelea na mazoezi katika kambi yao iliyopo Equator Grill jijini Dar es Salaam jana. Warembo hao wanataraji kupanda jukwaani leo katika ukumbi huo.
MACHAFUKO MTWARA
Hali ya usalama mkoani Mtwara ni tete. Mtu mmoja anaaminika kufariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa kutokana na vurugu kubwa zilizozuka jana huko Mtwara baada ya kusomwa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini na Nishati bungeni Dodoma jana.
Aidha, askari wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wamefariki dunia katika ajali wakitokea Nachingwea kwenda Mtwara ili kusaidia kutuliza vurugu hizo. Katika ajali hiyo, askari 20 walijeruhiwa, wengi wao vibaya na saba walinusurika.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Mohamed Kodi alithibitisha kupokea maiti moja na kuomba apewe muda kutaja idadi ya majeruhi.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa alidai kwamba hakuna mtu aliyefariki dunia wala majeruhi. Alisema watu 45 wamekamatwa.
Milio ya risasi za moto na mabomu ya machozi vilisikika kila kona na hasa Mitaa ya Mdenga, Magomeni na Shengena Mjini Mtwara ambako hali ilikuwa mbaya kutokana na kuwapo kwa mapambano kati ya polisi na vijana.
Vurugu hizo zilitokana na hatua ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kusisitiza kuwa bomba la gesi kutoka Mtwara na kuja Dar es Salaam litajengwa, jambo lingine linalodaiwa kusababisha ghasia hizo ni hatua ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutokurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge hivyo kuwakosesha wananchi fursa ya kusikiliza bajeti hiyo.
Akizungumzia kukosekana kwa matangazo hayo ya televisheni, Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana alisema kukatika kwa matangazo hayo kulitokana na tatizo la satelaiti katika mji huo na Musoma.
Hata hivyo, wakazi wa Mtwara waliokuwa na ving’amuzi walipata fursa ya kuangalia matangazo hayo.
Pia vurugu hizo zilichangiwa na vipeperushi vilivyosambazwa na watu wasiojulikana wakitaka watu kuacha kufanya shughuli zozote na kukaa nyumbani ili kufahamu hatima ya mradi wa usafirishaji wa gesi kutoka Msimbati hadi Dar es Salaam kwa njia ya bomba.
Katika vurugu hizo zilizozagaa zaidi maeneo ya Mikindani na Magomeni, wananchi pia waliharibu Daraja la Mikindani linalounganisha Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara.
Tangu asubuhi kama ilivyokuwa Mei, 17 mwaka huu, Mji wa Mtwara ulikuwa kimya na huduma nyingi za kijamii zilisimama ikiwamo usafiri wa pikipiki, daladala, mabasi maduka na masoko.
Wednesday, May 22, 2013
A MAN BEHEADED IN LONDON IN A HORRIFIC ATTACK
A man reported to be a serving soldier is dead and two people have been shot in Woolwich, south east London, after what Sky sources understand is being treated as a terrorist attack.
Downing Street has called a meeting of the Government's Cobra emergency committee after the incident in John Wilson Street, which David Cameron described as "truly shocking".
Sky sources understand that senior police officers believe the killing was likely to be a politically-motivated Islamist terrorist attack.
Dozens of weapons - including a number of knives - and pools of blood could be seen on the ground, where a man wearing a Help for Heroes T-shirt is said to have been attacked by two men.
![]() |
Witnesses say the pair appeared to deliberately drive their car at the victim, before getting out with various bladed weapons and launching their attack.
Sky sources say that following their attack, as the victim lay motionless in the middle of the road, witnesses heard the pair chanting "Allahu akbar" - and asking passers-by to take photographs of them.
Armed officers arrived at the scene and opened fire on the two alleged attackers. The men were taken to separate hospitals with gunshot wounds.
The Metropolitan Police confirmed one person had died following the incident and said the Independent Police Complaints Commission had now taken over the investigation.
Photographs taken at the scene show three people lying on the ground. Their condition was not clear. A car that appeared to have crashed could also be seen.
Commander Simon Letchford, from the Met, said officers were called to the road at 2.20pm.
"One man was being assaulted by two other men," he said.
"A number of weapons were reportedly being used in the attack, and this included reports of a firearm.
"Officers including local Greenwich officers arrived at the scene and shortly after firearms officers arrived on the scene.
"On their arrival at the scene they found a man, who was later pronounced dead. At this early stage I am unable to provide any further information about the man who has died.
"Two men, who we believe from early reports to have been carrying weapons, were shot by police. They were taken to separate London hospitals, they are receiving treatment for their injuries."
The Prime Minister is expected to cut short a trip to Paris to return to London in the wake of the incident.
Nigel Foran, who saw the incident as he returned home from shopping, described a scene of a confusion.
He told Sky News: "We saw a man running towards the police officers and then we heard a couple of gunshots.
"He went to the floor and was surrounded while officers drew their stun guns. After that, all the people who were watching ran away when they heard the gunshots."
The Ministry of Defence said it was urgently looking at the reports that the incident involved a soldier.
Greenwich and Woolwich MP Nick Raynsford had earlier told Sky News he believed the deceased was a serving soldier.
He said he had spoken to both borough commander Richard Wood and Lieutenant Colonel Bob Christopher at Royal Artillery Barracks - which is around a mile from the scene of the attack.
"We think a serving soldier was the victim. We don't know the circumstances surrounding the incident."
Schools in the area have been placed on lockdown.
Mayor of London Boris Johnson posted on his Twitter account: "This afternoon's attack in Woolwich is a sickening deluded and unforgivable act of violence."
Sourse: SKY NEWS
KIM KARDASHIAN SEVEN MONTHS PREGNANT PICTURES
She has admitted to struggling to adjust to the changes pregnancy has brought to her body.
But as she proudly showed off her bump in a simple bikini, Kim Kardashian proved she is finally at ease with her new shape.
Looking happy and healthy, her hair in braids and skin barely made up, the seven months' pregnant reality star was a true beauty.


ol


CREDITS: MAILONLINE
MTWARA HALI SII SHWARI
Mabomu ya machozi yalirindima na huduma zote za kijamii zilifungwa pamoja na usafiri, masoko, maduka na bar zote zilifungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazikufanya kazi.Mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kufuatia Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma hotuba yake Profesa Sospeter Muhongo alisema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam ndipo Wananchi wa Mtwara walicharuka! Daraja la Mikindani limevunjwa hakuna mawasiliano Mtwara na Dar es salaam.
Tuesday, May 21, 2013
SPOTTED ..............................................................
Before Miguel’s freak accident involving a fan at the Billboard Music Awards last night, he was all smiles as he hit the blue carpet with his fierce chick Nazanin. The lovely couple, dressed in all black, was also spotted at Tao Nightclub on Saturday for Maxim’s Music Weekend party.
Monday, May 20, 2013
FLAVIANA MATATA KUSHIRIKI MISA MAALUM KUHUSIANA NA WALIOPOTEZA MAISHA MV BUKOBA
Na Mwandishi Wetu
Mwanamitindo wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata leo atashiriki katika misa maalum ya kuwakumbuka watanzania waliopoteza maisha katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.
Misa hiyo itafanyika kwenye eneo la makabuli ya kumbukumbu ya MV Bukoba ambapo Flaviana alipoteza mama yake mzazi na kaka yake katika ajali hiyo.
Mwaka jana, mwanamitindo huyu kupitia shirika lake la Flaviana Matata Foundation alitoa msaada wa maboya yaani vyombo vya kuokoa maisha majini (life vests) 500 kwa mawakala wa meli ya serikali yaani Marine Services Ltd ikiwa ni nja moja ya kujaribu kusaidia usalama majini.
Mkurugenzi wa kampuni ya Compass Communications, Maria Sarungi alisema kuwa mbali ya kushiriki katika misa hiyo, pia mwana mitindo huyo atafanya mazungumzo na wadau mbali mbali jinsi ya kuendeleza juhudi za kuimarisha usalama majini.
Flaviana alisema kuwa juhudi zake kubwa kwa hivi sasa ni kuhakikisha kuwa ajali za vyombo vya kwenye maji zinaepukika na ndiyo maana anapigana huku na kule katika sakata hilo.
Alisema kuwa lengo lake kubwa ni kuona vyombo vya kuokolea katika kila meli vinapatikana na hasa kwa kutafuta misaada kwa wadau mbali mbali.
“Suala la usalama majini bado haujatiliwa mkazo vya kutosha na jamii pamoja na serikali” alieleza mwanamitindo huyu. “Muda umefika kwa wahusika wote kushirikiana kwa pamoja kuzungumzia na kukabiliana na changamoto hii” alisema Matata.
Sunday, May 19, 2013
MZEE ALLY SYKES AFARIKI DUNIA

FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES (PICHANI) KILICHOTOKEA LEO MEI 19, 2013 KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA, ALIKOKUWA AMELAZWA.
MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. MWILI WA MAREHEMU UNATARAJIWA KUWASILI JIJINI USIKU HUU.
MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA KESHO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.
HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.
Ø¥ِÙ†َّا Ù„ِÙ„ّÙ‡ِ ÙˆَØ¥ِÙ†َّـا Ø¥ِÙ„َÙŠْÙ‡ِ رَاجِعونَ
Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un. Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return.
Saturday, May 18, 2013
YANGA SC YAITUNGUA SIMBA SC 2-0
SHEREHE za Yanga kutwaa taji la 24 la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zimefana jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hiyo inafuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya watani wao jadi Simba SC katika mchezo wa kufunga pazia la ligi hiyo.
Kwa matokeo hayo, Yanga inamaliza msimu wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 60, ikifuatiwa na Azam FC yenye 52 na Simba 45
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na refa Martin Saanya wa Morogoro, aliyesaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililotiwa kimiani na Didier Kavumbangu dakika ya tano tu.
Kavumbangu alifunga kwa kichwa akiuwahi mpira wa juu uliopanguliwa na kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja kufuatia kona iliyochongwa na Haruna Niyonzima kutoka wingi ya kushoto. Mpira uliozaa kona hiyo ulitokana na Simon Msuva ambaye alikuwa anachanja mbuga, lakini beki Haruna Shamte akatoa nje.
Simba ilipata nafasi ya kusawazisha dakika ya 27 baada ya Mrisho Ngassa kuangushwa kwenye eneo la hatari na Nadir Cannavaro na refa Saanya kuamuru penalti, lakini mkwaju wa Mussa Mudde ulipanguliwa na Ally Mustafa ‘Barthez’ kabla ya kipa huyo kuuchupia na kuudaka.
Kwa ujumla, Yanga ilitawala kipindi ca kwanza karibu chote ingawa mwishoni mwa kipindi hicho, kidogo Haruna Chanongo aliitia majaribioni ngome ya Yanga kama mara mbili hivi na kusababisha kona mbili mfululizo.
Kipindi cha pili, Simba SC walikianza vizuri dakika 10 za mwanzo wakipeleka mashambulizi langoni mwa Yanga kutokea pembeni, lakini safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Bara ilisimama imara kukabiliana na hatari zote.
Krosi maridadi ya Simon Msuva dakika ya 62 iliunganishwa vyema kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego’ kuipatia Yanga bao la pili. Baada ya bao hilo, Yanga sasa walianza kucheza kwa kujiamini zaidi na Simba wakionekana kucheza ili kutoruhusu mabao zaidi.
Dakika 87 ya refa alijeruhiwa wakati anakwenda kuamua ugomvi kati ya Didier Kavumbangu na Nassor Masoud ‘Chollo’ akaanguka na kutibiwa kwa dakika hadi kuinuka dakika ya 90 na kumaliza mpira baada ya sekunde kadhaa.
Simba SC - Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Haruna Shamte, Mussa Mudde, Shomary Kapombe, William Lucian ‘Gallas’, Mrisho Ngassa, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme/Ranmadhani Singano ‘Messi’, Amri Kiemba/Jonas Mkude na Haruna Chanongo/Felix Sunzu.
Yanga SC - Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite/Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza/Niaar Khalfan.
KWA HISANI YA BIN ZUBEIRY
Hiyo inafuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya watani wao jadi Simba SC katika mchezo wa kufunga pazia la ligi hiyo.
Kwa matokeo hayo, Yanga inamaliza msimu wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 60, ikifuatiwa na Azam FC yenye 52 na Simba 45
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na refa Martin Saanya wa Morogoro, aliyesaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililotiwa kimiani na Didier Kavumbangu dakika ya tano tu.
Kavumbangu alifunga kwa kichwa akiuwahi mpira wa juu uliopanguliwa na kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja kufuatia kona iliyochongwa na Haruna Niyonzima kutoka wingi ya kushoto. Mpira uliozaa kona hiyo ulitokana na Simon Msuva ambaye alikuwa anachanja mbuga, lakini beki Haruna Shamte akatoa nje.
Simba ilipata nafasi ya kusawazisha dakika ya 27 baada ya Mrisho Ngassa kuangushwa kwenye eneo la hatari na Nadir Cannavaro na refa Saanya kuamuru penalti, lakini mkwaju wa Mussa Mudde ulipanguliwa na Ally Mustafa ‘Barthez’ kabla ya kipa huyo kuuchupia na kuudaka.
Kwa ujumla, Yanga ilitawala kipindi ca kwanza karibu chote ingawa mwishoni mwa kipindi hicho, kidogo Haruna Chanongo aliitia majaribioni ngome ya Yanga kama mara mbili hivi na kusababisha kona mbili mfululizo.
Kipindi cha pili, Simba SC walikianza vizuri dakika 10 za mwanzo wakipeleka mashambulizi langoni mwa Yanga kutokea pembeni, lakini safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Bara ilisimama imara kukabiliana na hatari zote.
Krosi maridadi ya Simon Msuva dakika ya 62 iliunganishwa vyema kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego’ kuipatia Yanga bao la pili. Baada ya bao hilo, Yanga sasa walianza kucheza kwa kujiamini zaidi na Simba wakionekana kucheza ili kutoruhusu mabao zaidi.
Dakika 87 ya refa alijeruhiwa wakati anakwenda kuamua ugomvi kati ya Didier Kavumbangu na Nassor Masoud ‘Chollo’ akaanguka na kutibiwa kwa dakika hadi kuinuka dakika ya 90 na kumaliza mpira baada ya sekunde kadhaa.
Simba SC - Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Haruna Shamte, Mussa Mudde, Shomary Kapombe, William Lucian ‘Gallas’, Mrisho Ngassa, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme/Ranmadhani Singano ‘Messi’, Amri Kiemba/Jonas Mkude na Haruna Chanongo/Felix Sunzu.
Yanga SC - Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite/Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza/Niaar Khalfan.
KWA HISANI YA BIN ZUBEIRY
Friday, May 17, 2013
HUDUMA MPYA YA USAFIRI WA RELI JIJINI DSM IKO NJIANI
Mh. Dk. Harrison Mwakyembe amesema wizara ya Uchukuzi inaangalia uwezekano wa kuanzisha huduma maalumu ya kati ya Stesheni ya Dar es Salaam na Gongo la Mboto kwa ajili ya kuhudumia abiria wanaoshukia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Dk Mwakyembe alisema hivi sasa wanatafuta mchakato wa kumpata mwekezaji na mwendeshaji wa huduma ya usafiri wa treni ya abiria katika jiji la Dar es Salaam.
“Mwekezaji huyo atatumia miundombinu ya reli iliyopo, vichwa vya treni na mabehewa maalumu kwa ajili ya usafiri wa abiria katika Jiji,” alisema Dk Mwakyembe, ambaye Wizara yake imeomba Sh491,105,994,000 katika bajeti hiyo, Sh100,584,174 zikiwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh390,521,220,00 kwa shughuli za maendeleo.
Alisema usafiri wa reli Dar es Salaam umesaidia kupunguza idadi ya magari barabarani kwani abiria 14,000 wanaotumia reli hiyo kwa siku wangehitaji mabasi 467.
Alisema wizara yake imetenga Sh113.1 bilioni kwa ajili ya kukamilisha ununuzi wa vichwa vinane vya treni, mabehewa 22 ya abiria, mabehewa 274 ya mizigo na mabehewa 34 ya breki.
Wednesday, May 15, 2013
KUTOKA UBALOZINI HAPA UK ...............

MAAFISA WA UBALOZI WETU HAPA UINGEREZA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MH. CHABAKA KILUMANGA ( ALIYESHIKA MAUA)ALIYEKUA NAIBU BALOZI HAPA UK AMBAYE HIVI KARIBUNI AMECHAGULIWA NA MHESHIMIWA RAISI KUWA BALOZI WETU COMORO
Tuesday, May 14, 2013
REDD MISS IFM WAKO TAYARI
Warembo wa Redd’s Miss IFM wakiwa katika picha ya pamoja.
Meneja wa Kinywaji cha Redd's Victoria Kimaro katikati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam juu ya maandalizi ya shindano la Redd's Miss IFM 2013.
Mratibu wa Redd’s Miss IFM, Daniel Sarungi katika akizungumza na waandishi wa Habari jijini dar es salaam juu ya shindano la Redd's IFM linalotarajiwa kufanyika May 25,2013, kulia ni meneja wa Kinywaji cha Redd's Victoria Kimaro
PICHA YA LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais mstaafu wa Nigeria na Balozi wa heshima wa IITA Chief Olesegun Obasanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Benjamin William Mkapa katika picha ya pamoja na wadau wa maendeleo bnaada ya kuzindua rasmi jengo la sayansi katika kituo cha Taasisi ya Kimataiafa ya Kilimo cha Tropiki (IITA) Mikocheni jijini Dar es salaam leo Mei 13, 2013.Picha na IKULU
Monday, May 13, 2013
UZINDUZI WA MSIMU MPYA WA CLOUDS FM DODOMA WAFUNIKA

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ajulikanae kwa jina la Snura akiimba jukwaani wimbo wake unaotamba kwa sasa katika vituo vingi vya redio,uitwao Majanga,mbele ya maelfu ya watu waliofika kwenye uwanja wa Jamuhuiri jioni ya leo wakati wa kituo cha redio ya Clouds FM ilipokuwa ikizindua msimu wake mpya kwa wasikilizaji wake,uzinduzi huo ulikwenda sambamba na kufanyika kwa semina ya fursa kwa Watanzania.
Msanii mahiri wa Mashairi hapa nchini,Mrisho Mpoto akiwakuna vilivyo wakazi wa mji wa Dodoma alipowaangushia maneno kadhaa na umati kulipukwa na mayowe kila kona,ambapo Clouds FM wamezindua msimu wao mpya.
Maelfu ya Watu wakiwa ndani ya uwanja wa jamhuri wakijumuika kwa pamoja na wana Clouds FM walipokuwa wakizindua msimu wao mpya.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya a.k.a bongofleva katika miondoko ya Hip Hop,Izzo Bizziness akikamua kwa shangwe kubwa mbele ya maelfu ya wakazi wa mji wa Dodoma waliofika ndani ya uwanja wa Jamuhuri,walipokwenda kushuhudia uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds FM.
Mkurugenzi wa vipindi na Utafiti,Ruge Mutahaba akizungumza na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye ndani ya Uwanja wa Jamuhuri jioni ya leo,wakati tamasha la uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds FM likiendelea,Nape alifika uwanjani hapo kujionea shamrashamra mbalimbali zilizojumuisha maelfu ya watu.
Palikuwa hapatoshi uwanja wa jamhuri Dodoma .
Picha na Habari kwa hisani ya SHAFFI DAUDA
MH. RAIS DKT JAKAYA KIKWETE ATEUA MABALOZI WAPYA

Rais Jakaya Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Mabalozi Wapya kujaza nafasi zilizo wazi na kuanzisha Ofisi za Ubalozi nchini Uholanzi na Comoro. Aidha Mheshimiwa Rais amefanya uhamisho wa Balozi kutoka kwenye kituo kimoja.
Mabalozi wateule na aliyehamishwa kituo ni kama ifuatavyo:-
Bw. Wilson M. K. Masilingi;
Ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi. Bw. Masilingi ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, Arusha, (AICC) na aliwahi kuwa Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwaka 1995 – 2010. Aidha, katika kipindi cha mwaka 1998 – 2005 alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais mwenye dhamana ya masuala ya Utawala Bora.
Bw. Chabaka Faraji Ali Kilumanga, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Hadi uteuzi huu unafanyika, Bw. Kilumanga alikuwa Balozi Mdogo katika ofisi ya Ubalozi nchini Uingereza.
Bw. Modest Jonathan Mero, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva. Kabla ya uteuzi Bw. Mero alikuwa Afisa wa Mambo ya Nje Mwandamizi kwenye Ubalozi wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa, New York.
Kadhalika, Mheshimiwa Rais amemhamisha Balozi Philip Sang’ka Marmo kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China na kwenda Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani.
Mabalozi wateule na aliyehamishwa kituo ni kama ifuatavyo:-
Bw. Wilson M. K. Masilingi;
Ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi. Bw. Masilingi ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, Arusha, (AICC) na aliwahi kuwa Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwaka 1995 – 2010. Aidha, katika kipindi cha mwaka 1998 – 2005 alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais mwenye dhamana ya masuala ya Utawala Bora.
Bw. Chabaka Faraji Ali Kilumanga, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Hadi uteuzi huu unafanyika, Bw. Kilumanga alikuwa Balozi Mdogo katika ofisi ya Ubalozi nchini Uingereza.
Bw. Modest Jonathan Mero, ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva. Kabla ya uteuzi Bw. Mero alikuwa Afisa wa Mambo ya Nje Mwandamizi kwenye Ubalozi wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa, New York.
Kadhalika, Mheshimiwa Rais amemhamisha Balozi Philip Sang’ka Marmo kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China na kwenda Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani.
------MWISH0-----
(John M. Haule)
KATIBU MKUU,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.
12 MEI, 2013
Saturday, May 11, 2013
MAZISHI YA WALIOFARIKI KWENYE MLIPUKO KANISA KATOLIKI ARUSHA
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe
akiweka shada la maua katika moja ya makaburi hayo. (PICHA NA SEIF MANGWANGI)
baadhi ya majeneza yenye miili ya marehemu ikiwa kanisani tayari kuombewa
Thursday, May 09, 2013
LONDON IS THE WORLD MILLIONAIRES PLAYGROUND
While global financial meltdown and double-dip recessions have left many of us counting the pennies, it seems that the streets of London are still paved with gold for some.
The UK capital is home to more multimillionaires than any other city in the world according to new figures.
London boasts a staggering 4,224 'ultra-high net worth' residents - people with a net worth of more than $30million, or £19.2million.

Millionaires playground: London boasts the highest number of individuals worth more than £19million in the world

Super-rich: Areas such as Knightsbridge, picture, Mayfair and Kensington, where property prices are particularly expensive, are home to many of London's super-rich

Wealthy: London is now home to a staggering 4,224 multi-millionaires
Subscribe to:
Posts (Atom)






























