Wednesday, 18 November 2009
RIPOTI YA IDADI YA WATU DUNIANI
WANAUME KAMA MABINTI (VISERENGETI)
Kijana wa mjini, Mwilu Mwilola ‘Silvanus’ ambaye hivi karibuni alifumwa kitandani akiwa na Miss Mwanza 2006-07, Aunt Ezekiel kabla ya kutimuliwa na aliyekuwa mchumba wake, Sarah, anakuwa kipimo cha kwanza kwa sababu ‘ishu’ yake bado haijapoa.Silva, alifumwa akiwa na Aunt kitandani, wote wakiwa watupu kabla ya vurumai kuchukua nafasi, kwenye nyumba aliyokuwa anaishi, Kinondoni, jirani na Leaders Club, Dar es Salaam Alhamisi ya wiki iliyopita.Habari ya kufumaniwa iliandikwa kwa mara ya kwanza na gazeti hili, toleo lake la Jumamosi iliyopita kabla ya Ijumaa Wikienda kuandika ‘ishu’ ya Silva kutimuliwa na kuanza maisha upya, baada ya kunyang’anywa kila kitu na Sarah.Kwa ujumla, habari zilizothibitishwa na Sarah, ndugu pamoja na marafiki wa karibu, zinaeleza kuwa Silva alikuwa akilelewa na mchumba wake huyo wa zilipendwa na kuhudumiwa kwa kila kitu kabla ya kuachwa kwa aibu hapa ‘juzi-kati’.
‘Brazameni’ wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Chalz Baba’ naye yumo kwenye ‘listi’ baada ya hivi karibuni, mwanamke aliyekuwa akiishi naye, Mariam Ramadhan kumtimua kwa maelezo kuwa ni msaliti wa penzi lao.Mariam, alimtimua Chalz baada ya brazameni huyo kuangukia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ‘The History’.Awali, Mariam alikuwa anaishi na Chalz Masaki, Dar es Salaam lakini baada ya kumtimua, hivi sasa mwana-Twanga huyo ‘anaminya’ kwenye ‘geto’ lake, Kinondoni Block 41, Dar.
Mwanamuziki mwingine wa Twanga, Kalala Hamza Junior hasahauliki kwenye orodha, yeye akitajwa kuishi ‘kisupastaa’ mjini kutokana na fedha za mrembo wake, Mary.Mbali na fedha, kwa sasa Kalala Jr hajui taksi wala daladala, badala yake ‘anaosha’ jina mjini kwa gari la Mary aina ya Toyota Nadia.
Twanga inaendelea kubeba ‘listi’ ya wanaume wanaopenda kulelewa kwa kumnyooshea kidole mwanamuzi ‘The Powerful Vocalist’, Saleh Kupaza ambaye kwa muda mrefu aliishi kwa nguvu ya mke wake, Mama Ife kabla ya kutengana.Saleh na Mama Ife, walitengana mapema mwaka huu baada ya mwanamuziki huyo kufumaniwa akiwa na mwanamke mwingine gesti.Mama Ife, ndiye aliyetinga kwenye ofisi za gazeti hili na kueleza kuwa yeye na Saleh basi, kabla ya kutangaza ndoa na aliyekuwa Meneja wa Televisheni ya C2C, Bahati Singh.Baada ya kuachana, Saleh alitunga wimbo unaopatikana kwenye albamu ya Mwana Dar es Salaam, unaoitwa Sitaki Kupenda ikiwa ni stori ya kweli, akielezea machungu aliyoyapata baada ya kupewa kisogo na Mama Ife.
Mwimbaji na rapa ‘The Amazing Vocalist’, Msafiri Said ‘Diouf’ ni mwanamuziki mwingine wa Twanga ambaye anadaiwa kuwa na hulka za kulelewa, akihusishwa na kimwana anayeitwa Mary, ingawa penzi lao haieleweki liliishia njia gani.
Dogo anayefanya kazi na Bendi ya FM Academia hivi sasa, Hassan Shaban ‘TX Moshi Jr.’ yupo kwenye namba ya wanaume wa hulka hiyo, yeye akidaiwa kuwekwa kinyumba na muigizaji Shumileta.Inaelezwa kwamba hivi sasa TX Jr. hataki tena kuishi kwenye nyumba yao ya Keko, badala yake ameamua ‘kuminya’ na Shumileta, Tabata, huku akitanua mjini na gari la muigizaji huyo.
Risasi Mchanganyiko linazo ‘data’ kuwa muigizaji ‘Mwili Jumba’, Gladys Chiduo ‘Zipompa’ aliwahi kumuweka kinyumba mwanamuziki wa zamani wa Bendi ya Diamond Sound, Zola Ndonga ambaye aliondoka kama alivyoingia pindi walipotibuana.
Kizito wa Kundi la Wateule, Jaffari Ally Mshamu ‘Jaffarai’ anaingia mzima mzima kwenye namba ya wanaume wanaolelewa kutokana na uhusiano wake wa kimapenzi na Meneja Uhusiano wa Benki ya NMB, Shyrose Bhanji.Kwa ujumla, penzi la Shyrose na Jaffarai siyo stori kutokana na kuandikwa mno na vyombo vya habari na inadaiwa kuwa nidhamu ya mwana-Hip Hop huyo ndiyo inayosaidia uhusiano wao kudumu mpaka leo.Katika uhusiano wao, Jaffarai amekuwa akipata huduma zote muhimu kutoka kwa Shyrose ambaye kutokana na kukolea kwa kijana huyo, huwa haoni ubahili ‘kukata pochi’ kumuwezesha ‘handsome boy’ wake.
Rais wa Bendi ya Akudo Impact, Christian Bella ‘Obama’ naye anatajwa kuwepo, akielezewa kwamba hivi sasa anapata matunzo yote kutoka kwa mwanamke anayefahamika kwa jina moja la Lillian.
Rapa wa FM Academia, Kitokololo a.k.a Kuku, pia anaongeza idadi ya wanaume wenye majina mjini ambao wanaishi kwa kulelewa na mademu zao, yeye akiwa amewekwa kinyumba na mwanamke aliyemzidi umri ‘jimama’, Sinza White Inn, Dar.Kabla ya kuhamia kwa mwanamke huyo, Kitokololo alikuwa anaishi na jimama lingine, Kinondoni, Dar kabla ya kutimuliwa kutokana na tabia yake ya ulevi wa kupitiliza kugeuka kero kwa mpenzi wake huyo.Risasi Mchanganyiko, hivi karibuni liliongea na Kitokololo ambaye alikiri kuhamia kwa jimama huyo, White Inn lakini akajigamba kwamba akiwa hapo, ni yeye ndiye ‘hukata pochi’ kwa ajili ya matumizi.
Mtangazaji wa Kituo cha Channel 10, Benny Kinyaiya anaingia moja kwa moja kwenye ‘listi’ kutokana na ile ‘ishu’ yake ya kutimuliwa na jimama na kutupiwa vyombo, ambayo iliandikwa magazetini.Katika sakata hilo, ilidaiwa kwamba Benny alikuwa akiishi kwa jimama hilo ambalo liliamua kumhudumia kwa kila kitu, lakini baadaye mwanamke huyo alimtimua kama vile hamjui baada ya penzi kutumbukia nyongo.
SOURCE : GPL
‘Brazameni’ wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Chalz Baba’ naye yumo kwenye ‘listi’ baada ya hivi karibuni, mwanamke aliyekuwa akiishi naye, Mariam Ramadhan kumtimua kwa maelezo kuwa ni msaliti wa penzi lao.Mariam, alimtimua Chalz baada ya brazameni huyo kuangukia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ‘The History’.Awali, Mariam alikuwa anaishi na Chalz Masaki, Dar es Salaam lakini baada ya kumtimua, hivi sasa mwana-Twanga huyo ‘anaminya’ kwenye ‘geto’ lake, Kinondoni Block 41, Dar.
Mwanamuziki mwingine wa Twanga, Kalala Hamza Junior hasahauliki kwenye orodha, yeye akitajwa kuishi ‘kisupastaa’ mjini kutokana na fedha za mrembo wake, Mary.Mbali na fedha, kwa sasa Kalala Jr hajui taksi wala daladala, badala yake ‘anaosha’ jina mjini kwa gari la Mary aina ya Toyota Nadia.
Twanga inaendelea kubeba ‘listi’ ya wanaume wanaopenda kulelewa kwa kumnyooshea kidole mwanamuzi ‘The Powerful Vocalist’, Saleh Kupaza ambaye kwa muda mrefu aliishi kwa nguvu ya mke wake, Mama Ife kabla ya kutengana.Saleh na Mama Ife, walitengana mapema mwaka huu baada ya mwanamuziki huyo kufumaniwa akiwa na mwanamke mwingine gesti.Mama Ife, ndiye aliyetinga kwenye ofisi za gazeti hili na kueleza kuwa yeye na Saleh basi, kabla ya kutangaza ndoa na aliyekuwa Meneja wa Televisheni ya C2C, Bahati Singh.Baada ya kuachana, Saleh alitunga wimbo unaopatikana kwenye albamu ya Mwana Dar es Salaam, unaoitwa Sitaki Kupenda ikiwa ni stori ya kweli, akielezea machungu aliyoyapata baada ya kupewa kisogo na Mama Ife.
Mwimbaji na rapa ‘The Amazing Vocalist’, Msafiri Said ‘Diouf’ ni mwanamuziki mwingine wa Twanga ambaye anadaiwa kuwa na hulka za kulelewa, akihusishwa na kimwana anayeitwa Mary, ingawa penzi lao haieleweki liliishia njia gani.
Dogo anayefanya kazi na Bendi ya FM Academia hivi sasa, Hassan Shaban ‘TX Moshi Jr.’ yupo kwenye namba ya wanaume wa hulka hiyo, yeye akidaiwa kuwekwa kinyumba na muigizaji Shumileta.Inaelezwa kwamba hivi sasa TX Jr. hataki tena kuishi kwenye nyumba yao ya Keko, badala yake ameamua ‘kuminya’ na Shumileta, Tabata, huku akitanua mjini na gari la muigizaji huyo.
Risasi Mchanganyiko linazo ‘data’ kuwa muigizaji ‘Mwili Jumba’, Gladys Chiduo ‘Zipompa’ aliwahi kumuweka kinyumba mwanamuziki wa zamani wa Bendi ya Diamond Sound, Zola Ndonga ambaye aliondoka kama alivyoingia pindi walipotibuana.
Kizito wa Kundi la Wateule, Jaffari Ally Mshamu ‘Jaffarai’ anaingia mzima mzima kwenye namba ya wanaume wanaolelewa kutokana na uhusiano wake wa kimapenzi na Meneja Uhusiano wa Benki ya NMB, Shyrose Bhanji.Kwa ujumla, penzi la Shyrose na Jaffarai siyo stori kutokana na kuandikwa mno na vyombo vya habari na inadaiwa kuwa nidhamu ya mwana-Hip Hop huyo ndiyo inayosaidia uhusiano wao kudumu mpaka leo.Katika uhusiano wao, Jaffarai amekuwa akipata huduma zote muhimu kutoka kwa Shyrose ambaye kutokana na kukolea kwa kijana huyo, huwa haoni ubahili ‘kukata pochi’ kumuwezesha ‘handsome boy’ wake.
Rais wa Bendi ya Akudo Impact, Christian Bella ‘Obama’ naye anatajwa kuwepo, akielezewa kwamba hivi sasa anapata matunzo yote kutoka kwa mwanamke anayefahamika kwa jina moja la Lillian.
Rapa wa FM Academia, Kitokololo a.k.a Kuku, pia anaongeza idadi ya wanaume wenye majina mjini ambao wanaishi kwa kulelewa na mademu zao, yeye akiwa amewekwa kinyumba na mwanamke aliyemzidi umri ‘jimama’, Sinza White Inn, Dar.Kabla ya kuhamia kwa mwanamke huyo, Kitokololo alikuwa anaishi na jimama lingine, Kinondoni, Dar kabla ya kutimuliwa kutokana na tabia yake ya ulevi wa kupitiliza kugeuka kero kwa mpenzi wake huyo.Risasi Mchanganyiko, hivi karibuni liliongea na Kitokololo ambaye alikiri kuhamia kwa jimama huyo, White Inn lakini akajigamba kwamba akiwa hapo, ni yeye ndiye ‘hukata pochi’ kwa ajili ya matumizi.
Mtangazaji wa Kituo cha Channel 10, Benny Kinyaiya anaingia moja kwa moja kwenye ‘listi’ kutokana na ile ‘ishu’ yake ya kutimuliwa na jimama na kutupiwa vyombo, ambayo iliandikwa magazetini.Katika sakata hilo, ilidaiwa kwamba Benny alikuwa akiishi kwa jimama hilo ambalo liliamua kumhudumia kwa kila kitu, lakini baadaye mwanamke huyo alimtimua kama vile hamjui baada ya penzi kutumbukia nyongo.
SOURCE : GPL
Tuesday, 17 November 2009
FIESTA ONE LOVE NDANI YA ZENJ (NGOME KUU)
Monday, 16 November 2009
SHEREHE ZA UHURU WA TANZANIA UKEREWE
5th DEC 2009 TANZANIA INDEPENDENCE CELEBRATION IN LONDONBONGODJS PROUDLY PRESENTS CELEBRATION OF TANZANIA INDEPENDENCE DAY ON SAT 5TH DECEMBER 2009 @ THE PRESTIGEOUS LA ROYALE BANQUENTING SUITES 819-821 HIGH ROAD TOTTENHAM LONDON N17 8ER FROM 7PM-3AM FOR ONLY£15 COME AND ENJOY LIVE BAND BONGODJS ON THE MIX,PS PASS THE MESSAGE AROUND!SPECIAL NITE NOT TO BE MISSED!!!
SPONSORED BY
SWIFT FREIGHTS UK
TZUK.com & BONGOTIMES
Saturday, 14 November 2009
NOLLYWOOD ACTOR KIDNAPPED
'worst storm of the year' causes Chaos
Gale-force winds and heavy rain brought flooding and damage to Britain today as parts of the country were battered by gusts of up to 100mph.
The lighthouse at The Needles on the westernmost point of the Isle of Wight reported gusts of between 95mph and 100mph.
In West Sussex, fire crews were called to two lightning strikes, and motorists had to be rescued from cars in Dorset after getting caught in flash floods.
The Environment Agency has 24 flood warnings in force, with the majority in southern coastal regions.
Stephen Davenport, of MeteoGroup UK, said: 'This is the strongest storm we have had this year, but it is just an autumnal storm, and not untypical for this time of year
The lighthouse at The Needles on the westernmost point of the Isle of Wight reported gusts of between 95mph and 100mph.
In West Sussex, fire crews were called to two lightning strikes, and motorists had to be rescued from cars in Dorset after getting caught in flash floods.
The Environment Agency has 24 flood warnings in force, with the majority in southern coastal regions.
Stephen Davenport, of MeteoGroup UK, said: 'This is the strongest storm we have had this year, but it is just an autumnal storm, and not untypical for this time of year
HARUSI YA VERO NA MATHEW LEO

Wakitoka kanisani St.Joseph mara baada ya kufunga ndoa yao.Kwa picha zaidi bofya hapa www.michuzijr.blogspot.com
Friday, 13 November 2009
MAMA KIKWETE KWENYE SHOO YA UTEPE MWEUPE

Mke wa Rais mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) akimweleza jambo Balozi wa kimataifa wa Utepe na msanii na mwanamitindo wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe.
Na Anna Nkinda – MAELEZOJumla ya dola za kimarekani 10,000/= zimepatikana kutokana na mnada wa nguo ya kike iliyotolewa na msanii na mwanamitindo wa Kimataifa Naomi Campbell katika maonesho ya mavazi ya Relief Tanzania yaliyofanyika jana usiku katika ukumbi wa Movenpick jijjini Dar es Salaam.Maonesho hayo yaliandaliwa na Naomi Campbell ambaye ni Balozi wa Kimataifa wa Utepe Mweupe kwa kushirikiana na Mustafa Hassanali ambaye ni mwanamitindo wa hapa nchini kwa lengo la kukusanya fedha ili kutunisha mfuko wa Mtandao wa Utepe Mweupe (The White Ribbon Alliance).Akiongea mara baada ya maonesho hayo Campbell alisema lengo la kufanya maonyesho hayo ni kupata fedha ambazo zitatumika katika kampeni ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.Kuhusu wabunifu wa mavazi na wanamitindo wa hapa Tanzania alisema anaridhishwa na kazi zao na wanajitahidi kufanya kazi nzuri kwa ufasaha mkubwa na kwa kujituma.Aliendelea kusema kuwa anaipenda nchi ya Tanzania kwa sasabu inavivutio vingi kama vile mbuga za wanyama, visiwa vya Zanzibar, mito, milima, maziwa na Bahari ya Hindi huku akisisitiza kuwa si mara ya kwanza kuja Tanzania na ana wa kuendelelea kuja hapa nchini.Katika maonyesho hayo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na Mke wa Rais wa Zambia Mama Thandiwe Banda walihudhuria.Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon Alliance) wenye takribani nchi wanachama 143 duniani ambao jana uliadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake unafanya kazi kubwa yakuhakikisha kuwa nchi wanachama zinaondokana na vifo vya kina mama wajawazito wakati wa kujifungua.
Na Anna Nkinda – MAELEZOJumla ya dola za kimarekani 10,000/= zimepatikana kutokana na mnada wa nguo ya kike iliyotolewa na msanii na mwanamitindo wa Kimataifa Naomi Campbell katika maonesho ya mavazi ya Relief Tanzania yaliyofanyika jana usiku katika ukumbi wa Movenpick jijjini Dar es Salaam.Maonesho hayo yaliandaliwa na Naomi Campbell ambaye ni Balozi wa Kimataifa wa Utepe Mweupe kwa kushirikiana na Mustafa Hassanali ambaye ni mwanamitindo wa hapa nchini kwa lengo la kukusanya fedha ili kutunisha mfuko wa Mtandao wa Utepe Mweupe (The White Ribbon Alliance).Akiongea mara baada ya maonesho hayo Campbell alisema lengo la kufanya maonyesho hayo ni kupata fedha ambazo zitatumika katika kampeni ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.Kuhusu wabunifu wa mavazi na wanamitindo wa hapa Tanzania alisema anaridhishwa na kazi zao na wanajitahidi kufanya kazi nzuri kwa ufasaha mkubwa na kwa kujituma.Aliendelea kusema kuwa anaipenda nchi ya Tanzania kwa sasabu inavivutio vingi kama vile mbuga za wanyama, visiwa vya Zanzibar, mito, milima, maziwa na Bahari ya Hindi huku akisisitiza kuwa si mara ya kwanza kuja Tanzania na ana wa kuendelelea kuja hapa nchini.Katika maonyesho hayo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na Mke wa Rais wa Zambia Mama Thandiwe Banda walihudhuria.Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon Alliance) wenye takribani nchi wanachama 143 duniani ambao jana uliadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake unafanya kazi kubwa yakuhakikisha kuwa nchi wanachama zinaondokana na vifo vya kina mama wajawazito wakati wa kujifungua.
APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO IKULU
SIMANZI WILAYANI SAME
SIMANZI na vilio jana vilitawala kwenye mazishi ya watu 2O waliofariki dunia kwa kufunikwa na kifusi kilichoporomoka mlimani na kufukia nyumba zao usiku wa manane katika Kata ya Mamba Miamba, wilayani Same, Kilimajaro.
watu zaidi ya 1,000 waliokusanyika katika msiba huo mkubwa wakiwa wamefunikwa na simazi, huku wakilia kwa uchungu kutokana na kupoteza ndugu zao katika mkasa huo wa kutisha.
Asilimia kubwa ya watu walionyesha masikitiko yao, hasa kwa familia ambayo imepoteza watu 15 na kati ya hao wanne hawajapatikana mpaka sasa.
Wanachi hao waliiomba serikali iwasaidie kutafuta miili ya watu hao na ikiwezekana watumie kikosi cha mbwa ili kubaini mahali ilipo.
Elineema Shambi, mmoja wa ndugu wa wanafamilia 15 waliofariki dunia na ambaye alinusurika kwa vile alikuwa amekwenda mjini Moshi kwa shughuli za kibiashara, alisema kwa majonzi kwamba amepoteza mke na watoto wake wanne ambao walifukiwa na kifusi hicho.
Alisema alikwenda mjini Moshi kununua bidhaa za kuuza, na kesho yake asubuhi alipigiwa simu na kuondoka mara moja. Alieleza kuwa alipofika alikuta nyumba yake imefunikwa kabisa kiasi cha kutoonyesha kama kulikuwa na nyumba na mwili wa mkewe ulikuwa haujapatikana hivyo akasaidia kuutafuta na kuupata pamoja na miili ya watoto wake.
Alifahamisha kuwa yeye ni mmoja kati ya ndugu wa watu 15 waliofariki katika tukio hilo la kutisha.
Akisimulia juu ya maporomoko hayo, alisema, dalili za mlima huo kuporomoka zilianza kuoneka mwaka jana kwa kuwa kulikuwa na ufa, hata hivyo hakueleza kwamba ni kwa nini hawakuhama katika eneo.
Akiunga mkono maelezo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega alibainisha kuwa wananchi wa Kata ya Mamba Miamba walishaona dalili za kuporomoka kwa mlima ulioua watu 20, tangu mwaka jana, lakini hawakuchukua tahadhari.
Wakati Mbega akisema hayo, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imesema haikuweza kutoa taarifa ya kutahadharisha wananchi dhidi ya janga hilo kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri mvua kubwa.
Mbega alitoa kauli hiyo jana katika eneo hilo la maafa wakati akiongoza maelfu kwa mamia ya wananchi wa eneo hilo na kutoka nje ya Wilaya ya Same katika mazishi ya watu waliofariki kutokana na janga hilo.
Mkuu huyo wa mkoa alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mlima huo ulianza kuonyesha ufa mwaka jana na baadaye Mei mwaka huu ufa huo ukazibika, lakini kumbe ndani ya mlima bado ulikuwa umeacha shimo kubwa.
Kwa mujibu wa Mbega, ambaye pia ni mbunge wa Iringa Mjini, pamoja na dalili zote hizo wananchi hao hawakuchukua hatua za tahadhari ikiwamo kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika ikiwamo serikali.
RC Mbega alisema endapo wananchi wangetoa taarifa mapema, serikali ingeweza kutuma wataalamu wake ambao wangesaidia kushauri jinsi ya kuepuka janga hilo.
Hadi kufikia jana saa 9:00 alasiri, miili ya watu wazima 19 na mtoto mchanga wa miezi tisa ilikuwa imeopolewa kutoka katika vifusi vilivyoporomoka kwenye mlima huo wenye majabali makubwa ya mawe.
Madaktari walilazimika kufanya upasuaji kwenye maiti ya mwanamke aliyejulikana kama Wemael Mhina, 30, ambaye ingawa siku zake za kujifungua zilikuwa zimeshatimia, hakujifungua hadi alipofikwa na mauti hayo.
Mkuu wa mkoa alisema Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika, Steven Wassira na Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Maua Daftari wametuma salamu za rambirambi.
Katika kuungana na wafiwa katika msiba huo mkubwa, Mbega alisema serikali imetoa Sh2 milioni za rambirambi kwa wafiwa na kugharamia shughuli zote za mazishi, ikiwa ni pamoja na chakula, malazi, matibabu na majeneza.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Ibrahim Marwa ameiomba serikali kutuma wataalamu wa miamba katika maeneo ya wilaya hiyo ili kuchunguza uhimili wake hasa kutokana na mvua nyingi zinazoendelea.
Marwa alisema tukio la kuporomoka kwa mlima liliwahi kutokea katika eneo la Hedaru, lakini halikusababisha madhara hivyo akasema upo umuhimu wa uchunguzi kufanyika.
Pia mkuu huyo wa wilaya aliuomba uongozi wa serikali na Jeshi la Polisi kutuma kikosi chake cha mbwa ili kusaidia kazi ya kutafuta miili ya watu wanne ambao wanaaminika bado wamenasa chini ya kifusi cha tope.
Marwa alisema mbwa hao watakuwa msaada mkubwa wa kubaini sehemu ambazo watakuwa wamefukiwa watu hao kutokana na mbwa hao kuwa na utaalamu na ujuzi wa kubaini mambo ya namna hiyo kwa kunusa.
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk Mathayo David ambaye pia ni mbunge wa Same Magharibi, alisema msiba huo ni mkubwa na kwamba umemgusa.
Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro isipokuwa Wilaya ya Siha, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya jirani,viongozi wa dini na wananchi.
Wakati wa mazishi hayo, kitongoji hicho cha Manja kilizizima kwa vilio na kwikwi kutokana na ukweli kuwa wengi waliofariki ni ndugu wa familia moja huku familia moja ikipoteza baba, mama na watoto wanne.
Eneo moja la makaburi kumezikwa ndugu tisa wa familia ambao walipoteza maisha katika tukio, wakati eneo jingine wamezikwa ndugu tisa wa familia moja huku eneo jingine wakizikwa ndugu wanne wa familia moja.
Shughuli za mazishi hayo zilianza saa 8:00 mchana na saa 9:15 alasiri ndipo waombolezaji walipoanza kazi rasmi ya kuzika huku simanzi kubwa ikionekana dhahiri miongoni mwa waombolezaji.
Wakati huohuo, Makoba Hassan na Thomas Ludovick wanaripoti kuwa TMA imesema haikuweza kuitahadharisha jamii kuhusu maafa yaliyotokea wilayani Same mkoani Kilimanjaro kwa sababu ya mvua kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri.
Kaimu Mkurugenzi wa shughuli za utabiri nchini, Matitu Mohammed alisema jana ofisini kwake kuwa hali hiyo ilitokea kutokana na vipimo vyao vya utabiri wa hali ya hewa wilayani hapo kuwa mbali na eneo lililotokea tukio hilo.
"Tukio lilitokea sehemu za milimani ambako vipimo vyetu vya utabiri vilishindwa kurekodi na kutoa taarifa kwa watu wa eneo hili kutokana na kituo chetu kuwa mbali," alisema Mohammed.
Alisema dhana kuwa mvua hizo ni El-Nino si ya kweli bali mvua hizo kitaalamu zinaitwa mvua za vuli ambazo hutokea katika kipindi hiki na husababishwa na ongezeko la joto katika Bahari ya Pacific
"Naomba wananchi waelewe kuwa hakuna mvua za El-Nino bali ni mvua za vuli ambazo huambatana na mfumo wa pepo zinazovuma kutoka Bahari ya Pacific kuelekea Bahari ya Hindi hivyo kusababisha mvua kubwa kutokea katika maeneo yote duniani," alisema.
Alizitaja sehemu zilizowahi kutokea maafa katika kipindi kilichopita kuwa ni Hedaru, Makanya, katikati ya Same na Mwanga na Same yenyewe kwa sasa ikiwa ni mara ya pili.
watu zaidi ya 1,000 waliokusanyika katika msiba huo mkubwa wakiwa wamefunikwa na simazi, huku wakilia kwa uchungu kutokana na kupoteza ndugu zao katika mkasa huo wa kutisha.
Asilimia kubwa ya watu walionyesha masikitiko yao, hasa kwa familia ambayo imepoteza watu 15 na kati ya hao wanne hawajapatikana mpaka sasa.
Wanachi hao waliiomba serikali iwasaidie kutafuta miili ya watu hao na ikiwezekana watumie kikosi cha mbwa ili kubaini mahali ilipo.
Elineema Shambi, mmoja wa ndugu wa wanafamilia 15 waliofariki dunia na ambaye alinusurika kwa vile alikuwa amekwenda mjini Moshi kwa shughuli za kibiashara, alisema kwa majonzi kwamba amepoteza mke na watoto wake wanne ambao walifukiwa na kifusi hicho.
Alisema alikwenda mjini Moshi kununua bidhaa za kuuza, na kesho yake asubuhi alipigiwa simu na kuondoka mara moja. Alieleza kuwa alipofika alikuta nyumba yake imefunikwa kabisa kiasi cha kutoonyesha kama kulikuwa na nyumba na mwili wa mkewe ulikuwa haujapatikana hivyo akasaidia kuutafuta na kuupata pamoja na miili ya watoto wake.
Alifahamisha kuwa yeye ni mmoja kati ya ndugu wa watu 15 waliofariki katika tukio hilo la kutisha.
Akisimulia juu ya maporomoko hayo, alisema, dalili za mlima huo kuporomoka zilianza kuoneka mwaka jana kwa kuwa kulikuwa na ufa, hata hivyo hakueleza kwamba ni kwa nini hawakuhama katika eneo.
Akiunga mkono maelezo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega alibainisha kuwa wananchi wa Kata ya Mamba Miamba walishaona dalili za kuporomoka kwa mlima ulioua watu 20, tangu mwaka jana, lakini hawakuchukua tahadhari.
Wakati Mbega akisema hayo, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imesema haikuweza kutoa taarifa ya kutahadharisha wananchi dhidi ya janga hilo kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri mvua kubwa.
Mbega alitoa kauli hiyo jana katika eneo hilo la maafa wakati akiongoza maelfu kwa mamia ya wananchi wa eneo hilo na kutoka nje ya Wilaya ya Same katika mazishi ya watu waliofariki kutokana na janga hilo.
Mkuu huyo wa mkoa alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mlima huo ulianza kuonyesha ufa mwaka jana na baadaye Mei mwaka huu ufa huo ukazibika, lakini kumbe ndani ya mlima bado ulikuwa umeacha shimo kubwa.
Kwa mujibu wa Mbega, ambaye pia ni mbunge wa Iringa Mjini, pamoja na dalili zote hizo wananchi hao hawakuchukua hatua za tahadhari ikiwamo kutoa taarifa kwa mamlaka zinazohusika ikiwamo serikali.
RC Mbega alisema endapo wananchi wangetoa taarifa mapema, serikali ingeweza kutuma wataalamu wake ambao wangesaidia kushauri jinsi ya kuepuka janga hilo.
Hadi kufikia jana saa 9:00 alasiri, miili ya watu wazima 19 na mtoto mchanga wa miezi tisa ilikuwa imeopolewa kutoka katika vifusi vilivyoporomoka kwenye mlima huo wenye majabali makubwa ya mawe.
Madaktari walilazimika kufanya upasuaji kwenye maiti ya mwanamke aliyejulikana kama Wemael Mhina, 30, ambaye ingawa siku zake za kujifungua zilikuwa zimeshatimia, hakujifungua hadi alipofikwa na mauti hayo.
Mkuu wa mkoa alisema Rais Jakaya Kikwete, Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika, Steven Wassira na Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Maua Daftari wametuma salamu za rambirambi.
Katika kuungana na wafiwa katika msiba huo mkubwa, Mbega alisema serikali imetoa Sh2 milioni za rambirambi kwa wafiwa na kugharamia shughuli zote za mazishi, ikiwa ni pamoja na chakula, malazi, matibabu na majeneza.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Ibrahim Marwa ameiomba serikali kutuma wataalamu wa miamba katika maeneo ya wilaya hiyo ili kuchunguza uhimili wake hasa kutokana na mvua nyingi zinazoendelea.
Marwa alisema tukio la kuporomoka kwa mlima liliwahi kutokea katika eneo la Hedaru, lakini halikusababisha madhara hivyo akasema upo umuhimu wa uchunguzi kufanyika.
Pia mkuu huyo wa wilaya aliuomba uongozi wa serikali na Jeshi la Polisi kutuma kikosi chake cha mbwa ili kusaidia kazi ya kutafuta miili ya watu wanne ambao wanaaminika bado wamenasa chini ya kifusi cha tope.
Marwa alisema mbwa hao watakuwa msaada mkubwa wa kubaini sehemu ambazo watakuwa wamefukiwa watu hao kutokana na mbwa hao kuwa na utaalamu na ujuzi wa kubaini mambo ya namna hiyo kwa kunusa.
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk Mathayo David ambaye pia ni mbunge wa Same Magharibi, alisema msiba huo ni mkubwa na kwamba umemgusa.
Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro isipokuwa Wilaya ya Siha, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya jirani,viongozi wa dini na wananchi.
Wakati wa mazishi hayo, kitongoji hicho cha Manja kilizizima kwa vilio na kwikwi kutokana na ukweli kuwa wengi waliofariki ni ndugu wa familia moja huku familia moja ikipoteza baba, mama na watoto wanne.
Eneo moja la makaburi kumezikwa ndugu tisa wa familia ambao walipoteza maisha katika tukio, wakati eneo jingine wamezikwa ndugu tisa wa familia moja huku eneo jingine wakizikwa ndugu wanne wa familia moja.
Shughuli za mazishi hayo zilianza saa 8:00 mchana na saa 9:15 alasiri ndipo waombolezaji walipoanza kazi rasmi ya kuzika huku simanzi kubwa ikionekana dhahiri miongoni mwa waombolezaji.
Wakati huohuo, Makoba Hassan na Thomas Ludovick wanaripoti kuwa TMA imesema haikuweza kuitahadharisha jamii kuhusu maafa yaliyotokea wilayani Same mkoani Kilimanjaro kwa sababu ya mvua kwa kuwa vipimo vyake havikuweza kutabiri.
Kaimu Mkurugenzi wa shughuli za utabiri nchini, Matitu Mohammed alisema jana ofisini kwake kuwa hali hiyo ilitokea kutokana na vipimo vyao vya utabiri wa hali ya hewa wilayani hapo kuwa mbali na eneo lililotokea tukio hilo.
"Tukio lilitokea sehemu za milimani ambako vipimo vyetu vya utabiri vilishindwa kurekodi na kutoa taarifa kwa watu wa eneo hili kutokana na kituo chetu kuwa mbali," alisema Mohammed.
Alisema dhana kuwa mvua hizo ni El-Nino si ya kweli bali mvua hizo kitaalamu zinaitwa mvua za vuli ambazo hutokea katika kipindi hiki na husababishwa na ongezeko la joto katika Bahari ya Pacific
"Naomba wananchi waelewe kuwa hakuna mvua za El-Nino bali ni mvua za vuli ambazo huambatana na mfumo wa pepo zinazovuma kutoka Bahari ya Pacific kuelekea Bahari ya Hindi hivyo kusababisha mvua kubwa kutokea katika maeneo yote duniani," alisema.
Alizitaja sehemu zilizowahi kutokea maafa katika kipindi kilichopita kuwa ni Hedaru, Makanya, katikati ya Same na Mwanga na Same yenyewe kwa sasa ikiwa ni mara ya pili.
Monday, 9 November 2009
LADYZZZZZZZZZ...
Singer Frenchie Davis and actress Kim Coles attended the 12th Annual GLAAD Tidings Season’s Greenings with Kim in a figure flattering all black outfit punctuated by a sequin tank, and Frenchie in a peachy pink wrap dress and gold sandals. Kim looks hot and sophisticated in her chic outfit and bow front sandals, but hmm, Frenchie…I don’t think the peak-a-boo lace bra works here. She certainly look saucy, but perhaps this dress would have benefited from either a lower cut bra or a cute comfy camisole.UMEME WA IPTL WAINGIZWA KWENYE GRIDI YA TAIFA
HATIMAYE mtambo mmoja kati ya mitambo 10 ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), umewashwa na kuanza kuingiza mewagati za umeme 10 katika gridi ya Taifa.Akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Dk. Magesvaran Subramanian, alikiri kuwashwa kwa mtambo huo na kuongeza kuwa uliwashwa rasmi jana saa 6.04 mchana.“Tumeanza kufanya kazi na mtambo mmoja namba moja ndio uliowashwa na mpaka sasa kila kitu kinakwenda vizuri tunatarajia mpaka kesho (leo), utakuwa umeshaanza kuzalisha megwati zote kumi,” alisema Dk. Subramanian.Naye Mfilisi wa kampuni hiyo, Rugonzibwa Mujunangoma, alisema mtambo huo uliwashwa jana, lakini kwa wakati ule haukuweza kuzalisha umeme wote wa megawati 10 na kwamba kadri ulivyokuwa ukiendelea kuzalisha umeme, ndipo megawati zilipokuwa zikiendelea kupanda na kufika 10.“Tangu mtambo uwashwe na hadi ninaondoka muda wa saa saba mchana, mtambo tayari ulishaanza kuingiza megawati 1.5, lakini hadi kesho (leo)), utakuwa tayari unazalisha megawati kumi, ikumbukwe hii ni mashine,” alisema Rugonzibwa.Kuhusu mitambo mingine tisa, alisema mafundi na watalaamu wa masuala ya umeme wanaendelea na ukaguzi ambapo nayo haitochukua muda mrefu itawashwa wakati wowote.“Kuwaka kwa mtambo huu ni dalili nzuri kuwa mitambo mingine nayo haitochukua muda itawaka, mafundi wanaendelea vizuri na kazi yao na kwa kweli hali inatia matumaini,” alisema mfilisi huyo.Kampuni hiyo ya IPTL ina mitambo 10 ambayo kila mmoja ukiwaka utatoa megawati 10 na hivyo mtambo mzima wa IPTL unatarajiwa kutoa megwati 100, na hivyo kupunguza tatizo la mgawo wa umeme ambalo limeikumba nchi kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Kihansi na Songas.Rais Jakaya Kikwete aliagiza katikati ya mwezi uliopita kwa mamlaka husika kuwa mitambo hiyo ya IPTL iwashwe ifikapo Novemba mosi, mwaka huu ili kukabiliana na tatizo la mgawo. Imechelewa kuwashwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kuchelewa kwa malipo kwa taasisi zitakazohusika kuendesha mitambo hiyo.
Sunday, 8 November 2009
USIKU WA MAGITAA CLUBAFRIQUE
MOTO WATEKETEZA "MAISHA CLUB" OYSTERBAY
Kiota cha kujiachia cha Maisha Club kilichopo Oysterbay jijini Dsm leo mchana kimeteketea kwa moto, taarifa zilizopatikana kutoka kwa mashuhuda wamesema kuwa kulikuwapo na ukarabati uliokuwa unaendelea wa vipupwe (AC),kwa bahati mbaya wakati wa ukarabati huo mojawapo ikalipuka kutokana na nyaya zake kugusana,na baadaye moto mkubwa ukazuka katika jengo hilo,imeelezwa kuwa taarifa zilifika kwa watu wa zima moto lakini hawakuwahi kuuzima moto huo kwa haraka kwani kwa asilimia kubwa vitu vilivyokuwemo vilikuwa vimekwishateketea.Saturday, 7 November 2009
Friday, 6 November 2009
HOUSE FOR SALE
WITO SHELUKINDO ATUTOKA DUNIANI
MALUMBANO CCM
MALUMBANO makali yameendelea kuitikisa Kamati ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi baada ya makombora ya juzi kuelekezwa kwa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango na mumewe, mzee John Malecela.
Kamati hiyo imekuwa ikipokea mashambulizi makali baina ya wabunge ambao wanaonekana kuwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi na wale ambao wanaona kuwa vita hiyo inawalenga, kiasi cha kurushiana tuhuma nzito zilizo na mwelekeo wa kuchafuana.
Baada ya kulipuana Jumanne, juzi ilikuwa zamu ya Mama Kilango na mumewe Malecela wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alipotoa tuhuma nzito akidai kuwa wawili hao pia wamekula fedha za ufisadi.
Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Simba alidiriki kudai kuwa hata harusi ya makamu huyo wa zamani wa CCM na Kilango ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel.
Patel kwa sasa ana kesi katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kuiibia Benki Kuu (BoT) kwa kuchota takribani Sh11 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).
Akijieleza kwenye kamati hiyo, Simba alimtuhumu Malecela, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, kuwa wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005, Jeetu Patel alimpa Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni zake.
Malecela, ambaye wakati huo alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM, aliondolewa mapema kwenye mbio za urais, ikiwa ni mara ya pili baada ya kuenguliwa tena mapema mwaka 1995.
Waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora akiwa na taasisi nyeti kama Takukuru na Idara ya Usalama wa Taifa, alizidi kurusha makombora kwa wanandoa hao, akisema Mama Kilango ni mnafiki na sio msafi kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole wakati harusi na kampeni zake za ubunge zilifadhiliwa na mtuhumiwa huyo wa ufisadi.
Habari zinasema kuwa Mama Simba alikuwa akizungumza kwa kujiamini na kwa ujasiri na kumtuhumu Mama Kilango kuwa kelele zake zote zinatokana na nongwa ya â€Å“kuukosa U-first lady (kuwa mke wa rais).
Alieleza kuwa kelele zote za mbunge huyo wa Same Mashariki zinatokana na chuki na uchu wa madaraka na si kweli kwamba ni mpinga ufisadi, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Lakini Patel, alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo za Waziri Simba kwamba alifadhili harusi ya Malecela na kampeni zake za urais, alionekana kustuka na kusema: "Haa...we nani kakwambia... Bwana ehee, mimi sijui lolote kuhusu hayo.
"Kwa sasa mimi najiangalia mwenyewe, nina matatizo yangu mengi nahangaika nayo."
Hata alipofafanuliwa kwamba, maneno hayo yalisemwa na Waziri Simba, alijibu: "Kama wao wamesema wenyewe huko, mimi sijui."
Naye Kilango alisema alishuhudia wakati wakati makombora hayo yakirushwa na kueleza kwamba anajiandaa kujibu mapigo.
Mbunge huyo machachari alisema anajua kwamba mambo yote yaliyosemwa, yanamlenga yeye na si mumewe Malecela.
"Mimi ni mwanasiasa... andikeni yote yaliyozungumzwa bila ya kuacha baadhi na siwezi kuwashtaki," alisema Kilango.
Mzee Malecela hakutaka kuzungumzia lolote kuhusu tuhuma hizo wakati alipoulizwa juu ya uhusiano wake na Patel na kama aliwahi kupokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kampeni.
"Ahaa... kijana naomba uniache nipumzike," alisema Malecela.
Mbali na mzee Malecela na mkewe, Waziri Simba pia alimgeukia mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akimtuhumu kuwa anaendesha vyombo vya habari vinavyoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi.
Pia alimshambulia mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akiwatuhumu kuwa ni watu wenye njaa na kwamba, wanalipwa fedha kufanya kazi hiyo.
Waziri Simba alisema kuwa hata tuhuma dhidi ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, zimetokana na chuki binafsi.
Simba alisema kuwa uchunguzi wa kashfa ya rada ulishamalizika na Chenge akasafishwa na kuongeza kwamba hata uchunguzi wa Richmond umebaini kulikuwa hakuna rushwa, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Suala la Richmond liliibuka tena mbele ya kamati hiyo ya Mwinyi wakati mbunge wa Bukoba Vijijini, Nazir Karamagi alipolalamika kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyoozwa Dk Mwakyembe haikumtendea haki.
habari hizo toka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Karamagi alisema ripoti ya Richmond ilionea baadhi ya watu na akapendekeza iundwe tume huru kupitia mchakato huo kuona kama wana makosa ili haki itendeke.
Mbunge huyo ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya Lowassa kuachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kashfa hiyo, alisema maamuzi yake kuhusu Richmond yalitokana na mapendekezo ya Bodi ya Tanesco.
Naye Dk Mwakyembe alijibu hoja iliyotolewa Jumanne na mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga aliyedai kuwa ripoti ya Richmond ni 'feki', akisema tatizo la Dk Mahanga ni uelewa mdogo.
Kuhusu hoja ya Karamagi, Dk Mwakyembe alisema malalamiko yake si sahihi kwa sababu yapo maeneo mengi ambayo Karamagi alishiriki na yako bayana hayahitaji mjadala.
Aliwatahadharisha Wabunge kuacha kudodosa sana ripoti ya Richmond kwani watazidi kumchafua Lowassa na kwamba wanaweza kufungwa kwa sababu upo ushahidi dhahiri.
Dk Mwakyembe aliwataka viongozi wa CCM wenye tuhuma kuiga mfano wa Mzee Mwinyi aliyejiuzulu baada ya mauaji yaliyofanywa na vyombo vya dola mkoani Shinyanga.
Akizungumza mbele ya kamati hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, alimshambulia spika wa Bunge, Samuel Sitta akidai kuwa kama si mizengwe, suala la Richmond lingemalizwa kwa taratibu za kichama.
Habari hizo zinadai kuwa Chenge, aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, alisema Lowassa alizungukwa na kwamba kulikuwa na njama za kummaliza ingawa hakusema njama hizo zilifanywa na nani.
Chenge aliitetea serikali ya awamu ya tatu kuhusu kuingia mikataba mibovu na kusisitiza hakukuwa na uzembe kwani mikataba yote ilipitiwa na kukubaliwa na Baraza la Mawaziri.
Hata hivyo, mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi alisimama na kuomba kutoa taarifa na kumwomba Mzee Mwinyi na kamati yake wawabane wabunge wanaodai wanasema ukweli.
Masilingi alipinga maelezo ya Chenge kuhusu mikataba na kusisitiza kuwa maelezo yake yalijaa ushabiki na kusema Baraza la Mawaziri liliridhia mikataba kutokana na ushauri wake (Chenge).
Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya, ambaye aliwahi kupata umaarufu kwa kulipua kashfa, aliwataka wabunge wakubali matokeo kuhusu Ripoti ya Richmond ili taifa lisonge mbele badala ya malumbano yasiyokwisha.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Mzindakaya aliwataka wabunge wafahamu kuwa ripoti hiyo ilishapitishwa na Bunge na haiwezi kurejeshwa ianze tena upya.
Naye Dk Mlingwa (Shinyanga Mjini), alisema mpasuko unaoinyemelea CCM unatokana na chama hicho kuacha misingi yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na badala yake kinawakumbatia wafanyabiashara.
Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitumia nafasi yake kuomba maridhiano ya wabunge wa CCM, kujenga moyo wa kusameheana ili chama kisonge mbele.
Kamati hiyo imekuwa ikipokea mashambulizi makali baina ya wabunge ambao wanaonekana kuwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi na wale ambao wanaona kuwa vita hiyo inawalenga, kiasi cha kurushiana tuhuma nzito zilizo na mwelekeo wa kuchafuana.
Baada ya kulipuana Jumanne, juzi ilikuwa zamu ya Mama Kilango na mumewe Malecela wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alipotoa tuhuma nzito akidai kuwa wawili hao pia wamekula fedha za ufisadi.
Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Simba alidiriki kudai kuwa hata harusi ya makamu huyo wa zamani wa CCM na Kilango ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel.
Patel kwa sasa ana kesi katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kuiibia Benki Kuu (BoT) kwa kuchota takribani Sh11 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).
Akijieleza kwenye kamati hiyo, Simba alimtuhumu Malecela, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, kuwa wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005, Jeetu Patel alimpa Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni zake.
Malecela, ambaye wakati huo alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM, aliondolewa mapema kwenye mbio za urais, ikiwa ni mara ya pili baada ya kuenguliwa tena mapema mwaka 1995.
Waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora akiwa na taasisi nyeti kama Takukuru na Idara ya Usalama wa Taifa, alizidi kurusha makombora kwa wanandoa hao, akisema Mama Kilango ni mnafiki na sio msafi kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole wakati harusi na kampeni zake za ubunge zilifadhiliwa na mtuhumiwa huyo wa ufisadi.
Habari zinasema kuwa Mama Simba alikuwa akizungumza kwa kujiamini na kwa ujasiri na kumtuhumu Mama Kilango kuwa kelele zake zote zinatokana na nongwa ya â€Å“kuukosa U-first lady (kuwa mke wa rais).
Alieleza kuwa kelele zote za mbunge huyo wa Same Mashariki zinatokana na chuki na uchu wa madaraka na si kweli kwamba ni mpinga ufisadi, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Lakini Patel, alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo za Waziri Simba kwamba alifadhili harusi ya Malecela na kampeni zake za urais, alionekana kustuka na kusema: "Haa...we nani kakwambia... Bwana ehee, mimi sijui lolote kuhusu hayo.
"Kwa sasa mimi najiangalia mwenyewe, nina matatizo yangu mengi nahangaika nayo."
Hata alipofafanuliwa kwamba, maneno hayo yalisemwa na Waziri Simba, alijibu: "Kama wao wamesema wenyewe huko, mimi sijui."
Naye Kilango alisema alishuhudia wakati wakati makombora hayo yakirushwa na kueleza kwamba anajiandaa kujibu mapigo.
Mbunge huyo machachari alisema anajua kwamba mambo yote yaliyosemwa, yanamlenga yeye na si mumewe Malecela.
"Mimi ni mwanasiasa... andikeni yote yaliyozungumzwa bila ya kuacha baadhi na siwezi kuwashtaki," alisema Kilango.
Mzee Malecela hakutaka kuzungumzia lolote kuhusu tuhuma hizo wakati alipoulizwa juu ya uhusiano wake na Patel na kama aliwahi kupokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kampeni.
"Ahaa... kijana naomba uniache nipumzike," alisema Malecela.
Mbali na mzee Malecela na mkewe, Waziri Simba pia alimgeukia mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akimtuhumu kuwa anaendesha vyombo vya habari vinavyoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi.
Pia alimshambulia mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akiwatuhumu kuwa ni watu wenye njaa na kwamba, wanalipwa fedha kufanya kazi hiyo.
Waziri Simba alisema kuwa hata tuhuma dhidi ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, zimetokana na chuki binafsi.
Simba alisema kuwa uchunguzi wa kashfa ya rada ulishamalizika na Chenge akasafishwa na kuongeza kwamba hata uchunguzi wa Richmond umebaini kulikuwa hakuna rushwa, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.
Suala la Richmond liliibuka tena mbele ya kamati hiyo ya Mwinyi wakati mbunge wa Bukoba Vijijini, Nazir Karamagi alipolalamika kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyoozwa Dk Mwakyembe haikumtendea haki.
habari hizo toka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Karamagi alisema ripoti ya Richmond ilionea baadhi ya watu na akapendekeza iundwe tume huru kupitia mchakato huo kuona kama wana makosa ili haki itendeke.
Mbunge huyo ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya Lowassa kuachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kashfa hiyo, alisema maamuzi yake kuhusu Richmond yalitokana na mapendekezo ya Bodi ya Tanesco.
Naye Dk Mwakyembe alijibu hoja iliyotolewa Jumanne na mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga aliyedai kuwa ripoti ya Richmond ni 'feki', akisema tatizo la Dk Mahanga ni uelewa mdogo.
Kuhusu hoja ya Karamagi, Dk Mwakyembe alisema malalamiko yake si sahihi kwa sababu yapo maeneo mengi ambayo Karamagi alishiriki na yako bayana hayahitaji mjadala.
Aliwatahadharisha Wabunge kuacha kudodosa sana ripoti ya Richmond kwani watazidi kumchafua Lowassa na kwamba wanaweza kufungwa kwa sababu upo ushahidi dhahiri.
Dk Mwakyembe aliwataka viongozi wa CCM wenye tuhuma kuiga mfano wa Mzee Mwinyi aliyejiuzulu baada ya mauaji yaliyofanywa na vyombo vya dola mkoani Shinyanga.
Akizungumza mbele ya kamati hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, alimshambulia spika wa Bunge, Samuel Sitta akidai kuwa kama si mizengwe, suala la Richmond lingemalizwa kwa taratibu za kichama.
Habari hizo zinadai kuwa Chenge, aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, alisema Lowassa alizungukwa na kwamba kulikuwa na njama za kummaliza ingawa hakusema njama hizo zilifanywa na nani.
Chenge aliitetea serikali ya awamu ya tatu kuhusu kuingia mikataba mibovu na kusisitiza hakukuwa na uzembe kwani mikataba yote ilipitiwa na kukubaliwa na Baraza la Mawaziri.
Hata hivyo, mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi alisimama na kuomba kutoa taarifa na kumwomba Mzee Mwinyi na kamati yake wawabane wabunge wanaodai wanasema ukweli.
Masilingi alipinga maelezo ya Chenge kuhusu mikataba na kusisitiza kuwa maelezo yake yalijaa ushabiki na kusema Baraza la Mawaziri liliridhia mikataba kutokana na ushauri wake (Chenge).
Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya, ambaye aliwahi kupata umaarufu kwa kulipua kashfa, aliwataka wabunge wakubali matokeo kuhusu Ripoti ya Richmond ili taifa lisonge mbele badala ya malumbano yasiyokwisha.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Mzindakaya aliwataka wabunge wafahamu kuwa ripoti hiyo ilishapitishwa na Bunge na haiwezi kurejeshwa ianze tena upya.
Naye Dk Mlingwa (Shinyanga Mjini), alisema mpasuko unaoinyemelea CCM unatokana na chama hicho kuacha misingi yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na badala yake kinawakumbatia wafanyabiashara.
Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitumia nafasi yake kuomba maridhiano ya wabunge wa CCM, kujenga moyo wa kusameheana ili chama kisonge mbele.
Thursday, 5 November 2009
Wednesday, 4 November 2009
BARAFU KUYEYUKA MLIMA KILIMANJARO
Wanasayansi kutoka Marekani wamegundua kuwa theluji na barafu katika mlima mrefu barani Afrika, Kilimanjaro uliopo nchini Tanzania inayeyuka kwa kasi na huenda ikatoweka ndani ya miaka 20.Utafiti huo ambao umechapishwa katika jarida la Proceedings of the National Academy of Sciences, ulikuwa wa kwanza kujua kiwango cha barafu kilichopotea katika mlima huo. Umegundua kuwa tandiko kuu la barafu hiyo lilisinyaa kwa asilimia themanini na tano tangu mwaka 1912.Barafu nyingine ilisinyaa kwa zaidi ya asilimia hamsini katika kipindi cha miaka tisa iliyopita.Utafiti huo umebaini kuongezeka kwa joto la dunia huenda ikawa ndio sababu ya kuyeyuka kwa theluji hiyo.
KESI YA KINA MRAMBA -RAIS MSTAAFU ATAJWA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana ilielezwa kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa ndiye aliidhinisha mchakato wa kuiajiri Kampuni ya Alex Stewart uendelee kwa haraka.
Hayo yalielezwa mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na hakimu John Utamwa wakati Wakili Hurbet Nyange alipokuwa akimhoji shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Godwin Nyelo (48).
Nyelo ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na masuala ya Uchumi wa Wizara ya Nishati na madini ni shahidi wa kwanza kwa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni serikali inayowakabili Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja.
Hata hivyo shahidi huyo alisema Rais Mkapa alihusika katika kukubali mchakato huo uendelee haraka baada ya Wakili Nyange kumuonyesha dokezo na kumtaka asome sehemu ya dokezo hilo naye kufanya hivyo mahakamani hapo.
Dokezo hilo lilikuwa limeandikwa kutoka kwa Daniel Yona ambaye kwa wakati huo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Rais huyo wa serikali ya awamu ya tatu.
Hayo yalielezwa mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na hakimu John Utamwa wakati Wakili Hurbet Nyange alipokuwa akimhoji shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka Godwin Nyelo (48).
Nyelo ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na masuala ya Uchumi wa Wizara ya Nishati na madini ni shahidi wa kwanza kwa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wake katika kesi ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni serikali inayowakabili Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja.
Hata hivyo shahidi huyo alisema Rais Mkapa alihusika katika kukubali mchakato huo uendelee haraka baada ya Wakili Nyange kumuonyesha dokezo na kumtaka asome sehemu ya dokezo hilo naye kufanya hivyo mahakamani hapo.
Dokezo hilo lilikuwa limeandikwa kutoka kwa Daniel Yona ambaye kwa wakati huo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kwenda kwa Rais huyo wa serikali ya awamu ya tatu.
Tuesday, 3 November 2009
MZEE ALEX KUSAGA AFARIKI DUNIA

Mwenyekiti mtendaji wa Clouds Media Group,Bw Alex Kusaga ambaye ni baba yake mzazi na Joseph Kusaga,amefariki leo jioni nchini Afrika ya Kusini ambako alipelekwa kwa ajili ya matibabu. Kwa taarifa zaidi tutaendelea kuwajulisha kadiri ya zitakavyokuwa zinatujia.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMIN
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMIN
HOSEAH AKOLEZA MOTO
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah amekoleza moto wa mjadala wa Bunge kuhusu utendaji wa taasisi yake baada ya kujitokeza hadharani na kueleza kuwa hana mpango wa kujiuzulu.Na kama haitoshi, Dk Hoseah amesema wabunge hawamtaki, wapige kura za kutokuwa na imani naye, ikiwa ni siku mbili kabla ya Bunge kujadili taarifa ya serikali ya utekelezaji wa maazimio ya chombo hicho kesho, kama alivyoahidi Spika Samuel Sitta.
Katika maazimio hayo kuhusu kashfa ya utoaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development LLC, Dk Hoseah anatakiwa kuwajibishwa na mamlaka ya juu kutokana na taasisi yake kushindwa kubaini rushwa katika utoaji wa zabuni hiyo.
Hoseah, aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari ambao kila mmoja alipewa kipeperushi kinachotoa ufafanuzi wa athari za malipo yasiyostahili kwa watumishi wa umma na adhabu zake, alionekana ni mwenye jazba, msimamo na kujiamini, licha ya joto la uchunguzi huo na shinikizo la wabunge kutaka awajibishwe, kuwa juu.
Akijibu swali kwamba kwanini asijiuzulu ili kuonyesha uadilifu baada ya maafisa wenzake waandamizi wa serikali waliotajwa katika Richmond kung'oka, Dk Hoseah alianza kuhoji: "Kwanini unataka nijiuzulu.
"Sasa nakwambia, sina mpango wa kujiuzulu siwezi kujitia kamba eti ili nionekane mzalendo bila kosa, kwanini unataka nijiuzulu au unataka kuchukua nafasi yangu?"
Hadi sasa, serikali haijaeleza kama imeshawashughulikia maofisa waandamizi waliotakiwa kuwajibishwa na mamlaka za juu, lakini katika kipindi cha miezi michache iliyopita, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika na Arthur Mwakapugi, aliyekuwa katibu mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini walistaafu kwa mujibu wa sheria.
Kauli ya Dk Hoseah inakuja wakati Takukuru ikishutumiwa kuwa inaendesha uchunguzi kuhusu malipo ya posho mbili dhidi ya wabunge kwa lengo la kuwashughulikia wale ambao wamekuwa mstari wa mbele kutaka serikali imwajibishe kutokana na uhusika wake kwenye kashfa ya Richmond.
Kashfa hiyo ya Richmond tayari inaonekana kusababisha msuguano mkubwa kati ya Bunge na Serikali, kiasi cha kusababisha watendaji wakuu wa taasisi hizo kutofautiana misimamo.
Huku kukiwa na ongezeko la kilio cha kutaka awajibishwe, Dk Hoseah alisema: "Nihukumiwe kwa haki si kwa hisia. Kosa langu nini katika Richmond, taarifa ya pili ya azimio namba 20 la Kamati ya Nishati na Madini bungeni iko wazi... lakini nasema uchunguzi dhidi ya wabunge utaendelea na naomba watoe ushirikiano; waiache Takukuru ifanye kazi zake; waonyeshe uongozi wa mfano na uadilifu kama ambavyo wamekuwa wakipambana na ufisadi."
Kumbukumbu za Bunge (Hansard), kuhusu Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini ya Agosti mosi, kujibu taarifa ya serikali iliyotolewa Julai 25, inasema: "Mheshimiwa Spika, Azimio Na. 20, Serikali iendeshe uchunguzi maalum ili kubaini ukweli kama taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokeo ya uchunguzi kuhusu mchakato wa Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine.
"Na kama jalada halisi linalohusu kampuni ya Richmond lililokuwa BRELA liliharibiwa na kuwekwa jingine kwa lengo la kuficha ukweli. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa Serikali: Kamati ya Vyombo vya Dola imekamilisha uchunguzi wake kuhusiana na suala hili.
"Na imebainika kuwa, si kweli kuwa taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokea ya uchunguzi kuhusu mchakato wa suala la Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine kwa lengo la kuficha ukweli.
"Vile vile, taarifa ya kamati ya vyombo vya dola inaonyesha baada ya upelelezi na uchunguzi wa kina kufanyika wameridhika kuwa jalada halisi la Richmond lililokuwa BRELA halikuharibiwa na wala hakukuwa na jalada lingine lililowekwa kuficha ukweli wa jambo hili."
"...Maoni ya Kamati; Kamati inaridhika na taarifa hiyo."
Hoseah akitumia azimio hilo, alisema alibahatika kusoma kwa makini taarifa zote za kamati kuanzia ya kwanza na hiyo ya pili na kuhoji : "Sasa nijiuzulu kwa kosa lipi, watu mnihukumu kwa haki, au unataka kuchukua nafasi yangu (alimuuliza mwandishi wa gazeti hili)?"
Alisema kwa kipindi chote atakachokuwepo katika uongozi, atasisimamia sheria na hakuna aliye juu ya sheria na kuongeza: "Watu waache danganya toto, hakuna kisasi ni usimamizi na utekelezaji wa sheria tu."
Dk Hoseah alifafanua kwamba, tayari suala hilo la kuwajibishwa liko mamlaka ya juu (rais), hivyo ni vema wakasubiri maamuzi na kusisitiza kwamba, "uchunguzi huo utaendelea kwa hiyo waheshimiwa wabunge, wazee wangu toeni ushirikiano ili suala hili lisije kutufikisha pabaya, nchi hii ni ya amani".
Mkuu huyo alitumia mkutano huo kufafanua pia kwamba, uchunguzi huo haukumlenga mtu yeyote ambaye ni mjumbe wa kamati iliyochunguza kashfa ya Richmond, akisema: "Kwanini, mbona Mheshimiwa Zitto (Kabwe) tumemhoji, yeye alikuwa kamati ya Richmond?"
Hoseah alisema ombi la kufanywa uchunguzi huo ni la Bunge lenyewe kupitia barua ya Februari 26, 2008, ambayo ilimtaja yeye kwa jina ikimtaka afanye uchunguzi huo na kuhoji: "Kwa hiyo Bunge lenyewe linaweza kuandika barua kutaka kuwalenga watu fulani?"
Spika Sitta alishaeleza kuwa hafahamu lolote kuhusu uchunguzi huo na kuitaka serikali isitishe zoezi hilo, huku Waziri Mkuu Mizengo Pinda akieleza kuwa suala hilo linatokana na maagizo ya ofisi ya rais.
Hata hivyo, alisisitiza kwamba kinachofanyika ni uchunguzi na haimaanishi wabunge wamethibitika kula posho mara mbili na kuongeza: "Sasa si ndiyo vizuri,... kwanza tunawapa haki nao kuwasikiliza, maana inawezekana mwisho wa siku ikibainika ni taarifa feki."
Kuhusu malalamiko ya wabunge kudhalilishwa na kuhojiwa na vijana wadogo wa taasisi hiyo, alipinga akisema si kweli na kuongeza: "Afisa ambaye anasimamia jambo hili ni mchunguzi mkuu ambaye amekuwa katika fani hii tangu mwaka 1973... kwa umri alionao hadi sasa anatarajia kustaafu mwakani."
Hata hivyo, awali akijibu maswali mengine, kama tatizo ni baadhi ya wabunge hawataki kuona sura yake (Hoseah) basi ni vema wakapiga kura ya kutokuwa na imani naye.
"Kama ulivyosema tatizo ni Hoseah hawajadili Takukuru, basi kama hawataki kuona sura yangu wapige kura ya kutokuwa na imani na mimi," alisisitiza.
UMALKIA WA KISURA TANZANIA

Visura wanaowania Umalkia wa Kisura wa Tanzania, juzi waliingia kambini katika hoteli ya Kiromo iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani wikiendi hii na kupokelewa kwa shangwe na wenyeji wao. Akizungumza hotelini hapo, Meneja Mradi wa kampuni ya Beautiful Tanzanie Agency, Grace Kilembe, washiriki hao walipatikana kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara. Aliitaja mikoa iliyofanyiwa usaili na kuwapata washiriki hao walioingia kambini juzi ni Singida, Dodoma, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Arusha, Mara na Dar es Salaam ambapo waliwapata wasichana 20 wenye vigezo vya mashindano hayo.
Aliwataja wasichana hao na mikoa waliyotoka kwenye mabano ni Mwajabu Juma (Mwanza), Lucky Mwakatobe, Resson Soto (Arusha), Jack's Oyombe, Alinda Lema, Violet Mganga, Sharon Silas (Dar es Salaam), Jackline Benson (Arusha) na Gloria Gilbert (Tanga). Wengine ni Glady Molel, Lightness Mwanga, Mwatatu Francis, Mary Joel, Shamim Babu (Manyara) na Mary Mallya (Dodoma), Asnat Mohammed na Diana Ibrahim (Mara).
Alisema washiriki hao watakaa katika kambi kwa muda wa mwezi mmoja na wiki mbili huku wakitoka mmoja mmoja mpaka watakapobaki 10 ambao wataingia fainali ya mashindano hayo. Grace alisema visura 10 watakaoingia fainali hiyo watapatikana kwa njia ya kupigiwa kura na watazamaji wa televisheni ya TBC1.
Mashindano ya Kisura wa Tanzania yamedhaminiwa na Serengeti Breweries Limited (SBL), Kiromo Resort, TBC1, Clouds FM, FHI, ATC, Entertainment Masters, Mwananchi Communication, Hugo Domino, Mercy G Parlor Beauty na Bang! Magazine. Grace alisema mwaka huu walijitokeza visura wengi katika hatua za awali tofauti na mwaka jana na kuwapa moyo waandaaji hao kuwa, wengi wameanza kuyaelewa mashindano hayo na manufaa yake.
Monday, 2 November 2009
Sunday, 1 November 2009
Saturday, 31 October 2009
SIMBA 1 YANGA 0
Habari zaidi tembelea www.issamichuzi.blogspot.com
SIMBA NA YANGA UWANJANI LEO
Macho na masikio ya maelfu ya mashabiki wa soka nchini leo yataelekezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara kati ya vigogo vya soka hapa nchini Simba na Yanga.
Huo utakuwa ni mchezo wa pili kwa vigogo hivyo kukutana ndani ya mwaka huu, ambapo mara ya kwanza ilikuwa ni Aprili 19 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja huo na timu hizo kwenda sare ya 2-2, ambapo Yanga ilikuwa na jukumu la kusawazisha.
Mchezo wa leo utakuwa na umuhimu mkubwa kwa Yanga kutokana na ukweli ina changamoto kadhaa za kukabiliana nazo.
Kocha mpya, Kostadin Papic aliyechukua mikoba kutoka kwa Dusan Kondic atakuwa anakalia benchi la timu hiyo kwa mara ya kwanza wiki tatu zilizopita.
Pia Yanga yenye pointi 18 itakuwa na kibarua cha kupunguza kasi ya Simba, ambayo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 27 baada ya kushinda mechi zake tisa za mwanzo.
Mchezo wa leo utakuwa na umuhimu mkubwa kwa Yanga kutokana na ukweli ina changamoto kadhaa za kukabiliana nazo.
Kocha mpya, Kostadin Papic aliyechukua mikoba kutoka kwa Dusan Kondic atakuwa anakalia benchi la timu hiyo kwa mara ya kwanza wiki tatu zilizopita.
Pia Yanga yenye pointi 18 itakuwa na kibarua cha kupunguza kasi ya Simba, ambayo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 27 baada ya kushinda mechi zake tisa za mwanzo.
Kutokana na ukweli kuwa ikipoteza mchezo huo ina maana itazidi kutoa mwanya kwa Simba kuzidi kupaa katika msimamo wa ligi hiyo. Yanga itakuwa fursa kwao kuendeleza ubabe wa kuifunga Simba kwa mara ya pili kwenye uwanja huo kama ilivyofanya katika raundi ya kwanza ya Ligi Kuu msimu uliopita, ambako Yanga ilishinda bao 1-0, Oktoba 26,2008.
Katika mchezo huo, Simba itakuwa na kazi moja tu ya kuhakikisha wanaendeleza wimbi la ushindi kwenye michezo yake ya ligi pamoja na kutaka kuweka rekodi mpya ya kushinda michezo 10 mfululizo.
Katika mchezo huo, Simba itakuwa na kazi moja tu ya kuhakikisha wanaendeleza wimbi la ushindi kwenye michezo yake ya ligi pamoja na kutaka kuweka rekodi mpya ya kushinda michezo 10 mfululizo.
Akizungumzia mchezo huo, kocha wa Yanga, Kostadin Papic alisema kuwa mara baada ya kukirekebisha kikosi chake ana matumaini ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo.
Kwa upande wake, kocha wa Simba, Patrick Phiri aliweka wazi kuwa anachohitaji ni pointi tatu kutoka kwa Yanga na uhakika wa kuzipata pointi hizo anao.
Kwa upande wake, kocha wa Simba, Patrick Phiri aliweka wazi kuwa anachohitaji ni pointi tatu kutoka kwa Yanga na uhakika wa kuzipata pointi hizo anao.
Friday, 30 October 2009
Subscribe to:
Posts (Atom)






















.jpg)
.jpg)
.jpg)















