.

.

.

.

Friday, October 09, 2009

TUZO ZA MAMA KESHO JIJINI NAIROBI

Ikiwa imebaki siku moja kabla ya kufanyika tukio la kihistoria Africa Mashariki la MTV AFRICA MUSIC AWARDS (MAMA), leo wasanii maarufu wa bara la Afrika ambao wako jijini Nairobi, wameongea na waandishi wa habari na kuelezea hisia zao kuhusu MTV Africa na onesho la kesho. Wasanii hao ni pamoja na Nameless wa Kenya, Lira wa Afrika Kusini, MI wa Nigeria, Simani wa Ghana, 2Face wa Nigeria na D'Banj "The KOKO Master" ambaye leo, kama ilivyokuwa pale Club Billicanas Tanzania, alikuwa kivutio kwa jinsi ambavyo alikuwa mcheshi na kutoboa siri ya kule alikolipata jina la KOKO Master. Alisema jina hilo alipewa na Waingereza wakati alipokwenda kufanya shoo hivi karibuni...

No comments:

Post a Comment