.

.

.

.

Sunday, May 05, 2013

KANISA LA RC ARUSHA LASHAMBULIWA NA WAUMINI WENGI WAJERUHIWA


BREAKING NEWS ............


Leo kulikuwa na uzinduzi wa Parokia mpya ya Olasit mjini Arusha. Mgeni rasmi alikuwa Mwakilishi wa Papa toka Vatican. Kulikuwa na wageni wengi waliambatana na mwakilishi wa papa, wakiwemo maaskofu, mapadre na watawa kutoka mataifa mbalimbali.

Mtoto mmoja ameeleza kuwa aliona watu waliokuwa kwenye mini bus wakirusha kitu kuelekea kwenye mkusanyiko wa wakristo waliokuwepo kwenye ibada.

Taarifa zinaeleza kuwa eneo kubwa limetapakaa damu, watu wengi wamejeruhiwa. Inasadikiwa kuwa wapo waliokufa lakini haijathibitika. Muda huu vyombo vyote vya usalama vipo eneo la tukio.

Kwa update zaidi sikiliza Radio Mariahttp://streema.com/radios/play/6848.

Hivi sasa kuna taharuki kubwa, na kuna taarifa ya milipuko mingine, haijulikani kama ni ya washambuliaji au ya polisi, mbali na eneo la ibada.

Nawapeni pole nyingi waliokumbwa na mkasa huu, wakatoliki, wakristo wote na wanaolitakia amani Taifa letu.


Taarifa  kutoka mkoani Arusha  ambazo  mtandao  huu  umezipata  zinaeleza  kuwa  kuna mlipuko  mkubwa mfano  wa  bomu umejitokeza katika kanisa la RC Arusha na kujeruhi  baadhi ya waumini.

Mlipuko huo  unadaiwa  kusababisha taharuki  kubwa katika mji  wa Arusha na kuendelea  kuiweka nchi katika hali tete  zaidi .

mwandishi maalum  wa mtandao  huu  kutoka Arusha anasema  kuwa tukio hilo  limetokea katika parokia ya  Olasit  mjini Arusha na bado jitihada za uokoaji zinaendelea  kufanyika.

No comments:

Post a Comment