.

.

.

.

Friday, December 31, 2010

TONITE AT CLUB AMBASSADORS

BOBBY FARRELL FOUND DEAD



Bobby Farrell, frontman of the 1970s pop group Boney M, was found dead in his hotel bed in St. Petersburg on Thursday while on tour in Russia. He was 61.

Farrell was discovered by hotel staff after he failed to respond to a wakeup call. He had given a concert in St. Petersburg on Wednesday evening.

His agent, John Seine, said he had complained of breathing problems, but the cause of death has yet to be determined.

Boney M was put together by German singer and songwriter Frank Farian in 1974, and had a huge following in Europe, including the Soviet Union, in the 1970s.

Farrell, who was more a dancer and showman than a singer, was the male face of the group, which included three other West Indian session singers — Marcia Barrett, Liz Mitchell and Maizie Williams.

Farian had a hit with Baby Do You Wanna Bump? and created Boney M to support the song.

The group went on to have hits such as Daddy Cool, Sunny, By the Rivers of Babylon and a favourite in North America, Rasputin'.

Boney M had 38 top-10 hits, including 15 that hit No. 1 in Germany, where they were then based, including Brown Girl in the Ring and Mary's Boychild.

Farrell was born Alphonso Farrell on Oct. 6, 1949, in Aruba. He left home at 15 as a sailor, then worked as a DJ in Germany before being picked by Farian to front Boney M.

In 1978, Boney M was the first Western music group to perform in the Soviet Union. They sang for an audience of 2,700 Russians in Red Square after being invited by Soviet leader Leonid Brezhnev.

The original group broke up in 1986. Williams is also touring with a group referred to as Boney M.

Farrell had been performing as Bobby Farrell of Boney M with three female backup singers. He continued to perform Boney M hits, and a mixture of calypso and disco songs.

Farrell, who made his home in Amsterdam, had been scheduled to perform a New Year's Eve concert in Rome.

Thursday, December 30, 2010

KATUNI ZA LEO


THE WORLD TALLEST MODEL




The world's tallest model Amazon Eve is living the high life - travelling the globe showing off her giant frame.

Eve, 31, stands at 6 feet 8 inches in her bare feet and completely dwarfs all other models as these incredible pictures show.

And amazingly, before November last year, she was completely unknown until a magazine put her in a bikini on the front cover - turning her into a overnight sensation.

Eve, from Turlock, California, is now a full-time model and actress but she also wrestles with men for $400 an hour.

She credits her height to genes - saying her German and Dutch heritage is the reason why she is so tall.

She said: 'All the women in my family are tall.'

What's more, Eve wears a ladies size 14 shoe which makes shopping for footwear more than a little difficult.





GROOVEBACK JUMAMOSI HII @ THAI VILLAGE

Tuesday, December 28, 2010

ALIKIBA KUWASHA MOTO READING MWAKA MPYA 2011

BAADA YA KUWARUSHA WAKAZI WA MJI MKUU {LONDON} VILIVYO, JUMAMOSI HII ALIKIBA KUKAMUA NDANI YA MJI WA KUSOMA NDANI YA FACE CLUB READING KAMA ULIKOSA SHOW YA CLUB AMBASSADOR HII NDIO NAFASI YAKO £10 KABLA YA SAA SITA USIKU £15 BAADA YA SITA WOTE MNA KARIBISHWA
HABARI NDIO HIYO UKOSE UCHEKWE!!!!!!!

JAJI MKUU MPYA TANZANIA

Image
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akifurahia jambo na Jaji Mkuu mpya, Othman Chande (kushoto) pamoja na aliyekuwa Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan. Jaji Mkuu huyo aliapishwa kwenye Viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam. (Picha na Fadhili Akida)

Sunday, December 26, 2010

MAMBO YA RED RIBBON CHARITY GALA 2010 KATIKA PICHA










PICHA KWA HISANI YA Issa Muhiddin Michuzi

LIBENEKE JIPYA TOKA MARYLAND-WASHINGTON DC , U.S.A

www.swahilivilla.blogspot.com/

imeanzishwa mjini Washington Dc na inaendeleza kazi zake katika mji wa Maryland. Inatumia lugha ya kiswahili na kingereza ili kuhabarisha kuhusu maswala mbalimbali ya kijamii hasa katika ukanda wa Marekani mashariki na Afrika mashariki. Itakuwa inakuletea habari mbalimbali za kijamii, siasa, burudani,michezo nk. Nakaribisha maoni yenu. Wasiliana nasi kwa. Email:kijiko12@hotmail.com

Saturday, December 25, 2010

MATUKIOUK INAWATAKIA KRISMASI NJEMA WADAU WAKE WOTE DUNIANI

Leo ni siku ya Krismasi ambapo Wakristo wote duniani wanaungana kusheherekea kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Ni siku ambayo Biblia Takatifu inasema kuwa mtoto Yesu Kristo alizaliwa katika mji wa Daudi uitwao Bethelehemu katika mazingira magumu na ya kimasikini, ikiwa ni namna ya kuufundisha ulimwengu umuhimu wa kuishi maisha ya uadilifu na unyenyekevu.

Kwa Wakristo, siku hii ni fursa ya kutawanya na kueneza ujumbe wa upendo, amani na upatanifu. Ujumbe wa Krismasi hutoa nanga ya amani kwa wale wenye nia ya kujenga jamii katika misingi ya kiroho na uwajibikaji wa pamoja. Ujumbe wa kipindi cha Krismasi huwakumbusha Wakristo kote duniani umuhimu wa kujirudi na kuacha dhambi na kuwatendea mema binadamu wote.

Biblia Takatifu inasema kuwa chimbuko la ujumbe huo wa kikristo ni upendo wa Mungu aliyewaumba binadamu na wito wake wa siku zote wa kuwahimiza kuwapenda majirani zao kama wanavyojipenda wenyewe. Ni ujumbe rahisi na wenye maana nzito, ingawa Wakristo wengi hudhani kuwa ni mgumu sana kuutekeleza. Ndio maana kila sikukuu ya Krismasi inapowadia, viongozi wa dini ya Kikristo katika madhehebu mbalimbali, huwahimiza tena waumini wao kuonyesha upendo kwa watu wote na wakati wote pasipo kujali tofauti za dini, kabila na jinsi.

Lakini kama mafundisho ya dini zote yanavyotukumbusha mara kwa mara, matatizo mengi yanayozikabili serikali nyingi na watu wengi duniani kamwe yasingekuwapo iwapo kila mtu angemtendea mwenzake kama ambavyo yeye angetaka atendewe. Kuwapo machafuko katika nchi yoyote kwa sababu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kama ilivyo huko Somalia na Ivory Coast au kama ilivyokuwa Rwanda, Burundi, Liberia na Siera Leone ni matokeo ya ubinafsi na ubaguzi ambavyo ni vichochezi vikuu vya vurugu, chuki na vita.

Ni kwa sababu hiyo tunategemea kwamba viongozi wa madhehebu ya Kikristo katika ibada za misa zao leo watatumia fursa hii ya kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo kukemea maovu katika jamii yetu ambayo kimsingi ndio vyanzo vya ukosefu wa upendo na uvunjifu wa amani. Kwa mfano, rushwa inaendelea kutafuna misingi ya umoja, amani na mshikamano wa Watanzania kutokana na viongozi wetu kukosa uzalendo na upendo kwa nchi yao na watu wake.

Kwa sababu ya kutaka kutawala milele, watawala wetu wamekosa utashi wa kisiasa wa kuipa nchi yetu katiba mpya itakayokidhi matakwa na matamanio ya wengi ili kutuepusha na uwezekano wa kuwapo vurugu na maangamizi katika taifa letu siku za baadaye. Viongozi wa Kikristo wachukue fursa ya maadhimisho ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo leo kuwaombea watawala wetu wapate ufunuo ili waone umuhimu na wakubali kwa dhati kuanza mkakati wa kuandika katiba mpya haraka iwezekanavyo.

Sisi tunawatakia kila la kheri Wakristo wote na wananchi kwa ujumla katika kusheherekea siku hiyo, na tunatoa rai kwamba katika kufanya hivyo, wachukue tahadhari ili kuepuka maafa, hasa ajali za barabarani ambazo tayari zinachukua maisha ya watu wengi kila kukicha. Ajali nyingi hutokana na shamrashamra za aina nyingi ambapo watu hula na kunywa, lakini kama wasomaji watakavyoona katika makala tuliyoyachapisha katika ukurasa wa tatu wa toleo hili, viongozi kadhaa wa Kikristo wanaonya kuwa kusheherekea kunapaswa kutanguliwa na maana ya kiroho ya kuzaliwa kwa Kristo.

Ni imani yetu kuwa Wakristo watawaelewa viongozi wao hao wa kiroho wanaposema kuwa baadhi ya Wakristo wanapotoka kwa kuacha kusudi la msingi la kuzaliwa kwa Yesu Kristo ambao ni ukombozi na badala yake wanafanya sherehe kubwa za vyakula na vinywaji, na pengine kushiriki katika anasa ambazo kimsingi zinamchukiza Mungu.

Friday, December 24, 2010

TONITE XMASS EVE COME AND CELEBRATE WITH US AT THE LOUNGE IN BARKINGS' CLUB AMBASSADOR

TIME : 10pm - 6AM

CARTOON OF THE DAY

OPRAH WINFREY ..........................


Oprah Winfrey covers the latest issue of Parade, in which she opens up about her new network, her biggest fears, how she hates the word ‘brand’ and more.

In exclusives extras, she also shares her thoughts on Sarah Palin and talks about howMichael Jackson helped her take the risk with the network.

MGAO WA UMEME TANZANIA KWA MWEZI MZIMA WATANGAZWA

SHIRIKA la Umeme (Tanesco) limetangaza mgawo mpya na mkubwa wa nishati hiyo ambao utavifanya viwanda, maduka, ofisi na makazi kukosa umeme kwa kati ya masaa sita hadi 12 kwa muda wa mwezi mzima.Tangazo hilo la mgawo ambalo limekuja katika kipindi ambacho mjadala wa jenereta za kampuni ya Dowans ukiwa umeibuka tena, linatarajiwa kuongeza gharama za maisha kutokana na ukweli kuwa viwanda vingi vitalazimika kutumia jenereta katika uzalishaji licha ya Tanesco kutangaza kuwa vitapewa umeme nyakati za mchana.

Wananchi ambao kipato chao kinategemea biashara ya samaki, saluni, na vinywaji pia wataguswa na makali hayo moja kwa moja wakati mabenki, vituo vya mafuta, mahoteli na makampuni mengine ya kutoa huduma yatajikuta yakiingia gharama kubwa katika utendaji wao.

Tangazo la Tanesco limetolewa wakati kukiwa na ahadi kemkem za kumaliza kabisa tatizo la mgawo wa umeme, huku Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ikiwa imeliruhusu shirika hilo la umma kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 18.5.
"Mgawo huu wa umeme umeshaanza kwenye mikoa yote na utadumu kwa majuma manne hadi katikati ya mwezi Januari mwakani," alisema meneja mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud alipoongea na waandishi jana.
"Mgawo utahusisha mikoa yote iliyounganishwa kwenye gridi ya taifa isipokuwa mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Lindi na Mtwara."

Kwa mujibu wa Masoud, mgawo wa sasa umetokana na upungufu wa umeme uliojitokeza baada ya moja ya visima vinavyozalisha gesi vya kampuni ya Pan African Energy, kuzimwa.
Alisema kisima hicho kinachotoa gesi kimezimwa kwa ajili ya kukifanyia matengenezo ya kawaida, hivyo kusababisha upungufu wa megawati 40 za umeme zinazokwenda katika gridi ya taifa.

Pan African Energy ni kampuni ambayo inachimba gesi hiyo eneo la Songo Songo, Kilwa na baadaye husafishwa na kusafirishwa na kampuni ya Songas ambayo huzalisha umeme wa megawati 180 eneo la Ubungo na kuiuzia Tanesco.
Kwa mujibu wa makubaliano, Songas hutakiwa kuzalisha umeme kwa kiwango kilicho kwenye mkataba na ni jukumu la Tanesco kuutumia umeme huo wa gesi kulingana na mahitaji yake au kutoutumia. Tanesco huilipa Songas hata pale inapokuwa haitumii umeme wa kampuni hiyo.

Badra alisema kuwa kiwango hicho cha upungufu wa umeme kinaweza kuongezeka hadi kufikia megawati 120 jambo alilosema likitokea, shirikma hilo litazidisha mgawo.
“Wakati mwingine kunapokuwa na peak (matumizi yanakuwa makubwa), upungufu unaweza kufikia megawati 120. Ikitokea hivyo, kwa kuwa sasa tunategemea uzalishaji umeme kwa njia ya maji, itabidi nasi tuongeze mgawo,” alisema Badra.
Alieleza kuwa mgawo huo utaanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni katika baadhi ya maeneo huku maeneo yaliyopata umeme katika muda huo yakiukosa kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 5:00 usiku mara tatu kwa wiki.

Kwa mujibu wa Badra, ratiba ya mgawo huo zitatangazwa katika magazeti na vyombo vingine vya habari.
Hata hivyo, alisema baadhi ya maeneo hayatakumbwa na mgawo huo akitaja baadhi kuwa ni hospitali, pampu za maji, migodi na viwandani ambako alisema vitakosa umeme usiku ili mchana viendelee kuzalisha.
Alisema kuwa maeneo yanayopata umeme kutoka transoma ya Kipawa hawatakumbwa na mgawo huo, kutokana na kukamilika kwa matengenezo yake.

“Transfoma ya Kipawa imeshatengemaa na hivyo kuanzia Desemba 23 (jana) haki ya kupata umeme katika maeneo yaliyoathirika kutokana na kuharibika kwa transfoma hiyo, itarejea kama kawaida na wateja wa maeneo hayo hawatakumbwa na mgawo huu tulioutangaza,” alisema Badra.
Baadhi ya maeneo yanayopata umeme kutoka transfoma hilo ni pamoja na Yombo Dovya, Tandika, Temeke, Chang’ombe, Chamazi, Tazara, Maji Matitu, Charambe, Keko na Uwanja wa Taifa.

Akizungumzia siku kuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, Badra alisema Tanesco itajitahidi kuhakikisha wananchi wanasherehekea siku hizo bila kukosa umeme huku akiwaomba radhi kwa mgawo huo.

Mgawo wa umeme, ambao ulizalisha kashfa kubwa ya Richmond ulipoibuka mwaka 2006, umeshaanza kuzoeleka kwa wananchi na ahadi za shirika hilo na wizara kugeuza tatizo hilo kuwa historia, sasa zinaonekana za kawaida.
Machi 16 mwaka huu Tanesco ilitangaza mgawo wa umeme katika mikoa yote ya Tanzania Bara uliokuwa wa saa tano kila siku. Wakati mgawo huo ukiisha, Tanesco ilitangaza kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.
Watanzania, ambao ni asilimia 12 tu wanaotumia huduma hiyo majumbani, pia walipata machungu ya mgawo wa umeme Oktoba mwaka uliopita ambapo walikosa huduma hiyo kwa saa 12 kwa siku.

Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo Stephen Mabada, alitangaza mgawo huo akieleza kwamba Tanesco ililazimika kuanza mgawo huo kutokana na upungufu mkubwa wa uzalishaji umeme, uliosababishwa na kuharibika kwa mitambo minne kwenye vituo vya uzalishaji wa nishati hiyo.
Mitambo iliyoharibika ilikuwa ni ya Kidatu, mkoani Morogoro, Kihansi (Iringa) na Pangani (Tanga) wakati jijini Dar es Salaam mtambo wa kuzalisha umeme wa gesi asilia wa Songas pia uliripotiwa kuharibika.
Wakati huo, serikali iliamuru kuwashwa kwa mitambo inayozalisha umeme kwa kutumia mafuta ya IPTL licha ya kampuni hiyo na Tanesco kuwa kwenye mgogoro mkubwa ambao unashughulikiwa mahakamani.

Matatizo makubwa ya umeme yaliibuka mwaka 2006 wakati nchi ilipokumbwa na janga kubwa la ukame na ikabidi serikali ichukue hatua za dharura kumaliza tatizo hilo.

Lakini hatua hizo za dharura zikaishia kwenye kashfa kubwa ya utoaji zabuni ya uzalishaji umeme kwa kampuni ya Richmond Development LLC, ambayo ilidhihirika baadaye kuwa haikuwa na uwezo wa kutekeleza wajibu wake kwenye mkataba.
Baadaye mkataba huo ulirithishwa kwa kampuni ya Dowans Tanzania ambayo, licha ya kuchelewa, ilileta nchini mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi iliyokuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 120.
Lakini mwaka 2008 Tanesco ilikatisha mkataba huo mwaka mmoja kabla ya kumalizika, ikidai kuwa Sheria ya Manunuzi ya Umma ilikiukwa wakati wa kuingia mkataba huo, lakini ikaahidi kuwa ina uwezo wa kuzalisha umeme bila ya kutegemea jenereta hizo.

Uamuzi huo uliifanya Dowans kufungua kesi Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC), ikidai kuwa taratibu hazikufuatwa wakati wa kuvunja mkataba huo.
Mwaka mmoja baadaye Tanesco ikaibuka na hoja ya kutaka kuinunua mitambo hiyo ya Dowans, ikidai kuwa nchi ilikuwa hatarini kuingia kwenye tatizo kubwa la umeme na kwamba isingekuwa rahisi kununua mitambo mingine kabla ya tatizo hilo kuanza.

Hata hivyo, hoja hiyo ilipingwa vikali na Kamati ya Madini na Nishati ambayo ilieleza kuwa kununua mitambo hiyo mitumba ni kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma, kitu kilichomfanya mkurugenzi wa Tanesco wa wakati huo, Dk Idris Rashid kutoa tamko kuwa iwapo nchi itaingia gizani, asilaumiwe.

Mapema mwezi huu, ICC) ilitoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Dowans na kuiamuru Tanesco kuilipa kampuni hiyo binafsi fidia ya Sh185 bilioni.


Thursday, December 23, 2010

BAHARI BEACH HOUSE FOR RENT









Bathrooms : 4
Bedrooms : 5
Location: Bahari Beach, Dar-es-Salaam
Living Area (Sqm):
Plot Size (Sqm): N/A
Asking Price: USD 1,000

contact;

Alex Mbaga+255-716-337-196
+255-786-725-734
+255-786-725-734

SPOTTED ...................................

One of this season’s hottest thing is trend- lace up boots! They have been spotted all over the runways, in your favorite stores & boutiques- and your favorite celebs are all over it. These boots are extremely versatile and you can find them as booties, mid calf, knee high, and thigh high! And if you aren’t into wearing 4 inch heels, you can also purchase lace up flats and still look hot

MISS ILALA 2010

Image
Mrembo wa Ilala 2010 Bahati Chando (wa pili kulia) pamoja na wageni mbalimbali aliofuatana nao wakipamba mti wa Krismasi na watoto wa Kituo cha Loveness ikiwa ni ishara ya kusherehekea nao kwenye kituo hicho. (Picha na Fadhili Akida).

Tuesday, December 21, 2010

KUNA NINI CHRISTMAS EVE ???



MGAO WA UMEME TENA

WAKATI Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), ikiamuru wafanyakazi takribani 5,000 wa Tanesco kulipa viwango sawa vya bei za umeme kama ilivyo kwa wananchi wengine, na ikiridhia kupandisha bei ya umeme kuanzia Januari mosi, mgawo wa umeme unaanza tena leo.

Mgawo wa umeme uliositishwa wiki moja iliyopita, umetangazwa jana mjini Kilwa mkoani Lindi ikiwa ni kutokana na Kampuni ya Pan African Energy inayozalisha gesi asili katika kisiwa cha Songosongo kupunguza uzalishaji kwa ajili ya kufanyia matengenezo kisima kimoja kati ya vitano ilivyonavyo.

Mahitaji ya matengenezo ya kisima hicho yaligundulika Septemba mwaka huu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba alisema Tanesco imelazimika kuanza tena mgawo tena kutokana na upungufu wa megawati 40, akisema “tunalazimika kupunguza uzalishaji katika mtambo wa Ubungo ambapo baada ya kuzalisha umeme wa megawati mia moja, sasa tutalazimika kuzalisha megawati 60, na ratiba tutartoa baada ya kuipanga.”

Mramba alitangaza mgawo huo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakati alipotembea Kilwa Kisiwani kunakozalishwa gesi asilia kwa ajili ya kuiuzia Tanesco na Kampuni ya Songas.

Akitoa taarifa kuhusu kukifanyia matengenezo kisima hicho, Naibu Meneja Mkuu wa Pan African Energy, William Chiume alisema kutokana na matengenezo hayo, watapunguza uzalishaji kwa asilimia 16 kutoka futi za ujazo milioni 86 hadi 76, ambazo ni sawa na megawati 40.

Alisema matengenezo hayo yatachukua kati ya wiki nne na tano kuanzia sasa. Hata hivyo, alisema waathirika wakubwa ni Tanesco, kwani Songas wataendelea kupata gesi kutokana na mkataba walionao. Songas pia wanaiuzia umeme Tanesco.

Songas inaiuzia Tanesco megawati 182 za umeme kwa siku na wakati mitambo ya Tegeta inazalisha megawati 45, Ubungo megawati 100, yote ya gesi asili wakati mahitaji ni megawati 833 kwa siku.

Wakati mgawo huo ukitangazwa Kilwa, jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Ewura, Haruna Masebu alitoa uamuzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Ewura wa maombi ya Tanesco ya kubadilishiwa bei za umeme, na kueleza kuwa Bodi imekubali ombi hilo na imepandisha bei ya umeme kwa asilimia 18.5 kuanzia Januari mosi.

Masebu alisema wafanyakazi hao wamekuwa wakilipia viwango maalumu, hivyo Bodi imeamuru walipe kama ambavyo wananchi wengine wanalipia na endapo hawatotekeleza itaonekana wakati wa ukaguzi.

Akifafanua zaidi, Mkurugenzi wa Umeme wa Ewura, Anastas Mbawala alisema wafanyakazi wa Tanesco wanakadiriwa kufikia 5,000 na wamekuwa wakilipa Sh nne kwa kila uniti ya umeme, ingawaje kwa wale ambao ni mke na mume, alikuwa anapewa mmojawapo na sio wote.

Kuhusu bei ya umeme, Masebu alisema maombi ya Tanesco yalitolewa Mei 28, mwaka huu na mchakato ulianza mara moja wa kukutana na wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili kwa kina suala hilo ili kila mmoja aridhike na hatua zitakazofuatia.

Masebu alisema mikutano ilifanyika Agosti katika mikoa ya Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro, Tabora na Dar es Salaam, na kwamba “baada ya kukutana na wadau mbalimbali na kujadili kwa kina suala la kubadilishiwa bei hizo, Ewura iliona kuna hoja ila hawawezi kukubali maombi hayo kama yalivyoletwa na Tanesco.”

Alisema Tanesco waliomba kuwe na mpangilio wa kubadilisha bei ya umeme kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka 2011 kwa asilimia 34.6, asilimia 13.8 na asilimia 13.9 ili waboreshe huduma zao na kuwa endelevu wakati wote.

Kadhalika alisema Tanesco waliomba pia mabadiliko hayo yaende pamoja na kuwa na uwezo wa kurekebisha viwango vya umeme wakati wowote, kuruhusiwa kubadilisha bei ya umeme katikati ya kipindi hicho kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta na kubadilika kwa viwango vya umeme kadri ya matumizi.

Alisema ni kweli Tanesco wanahitaji zaidi ya Sh bilioni 691 ili itoe huduma endelevu, hivyo Ewura imekubali ombi lao kwa asilimia 18.5 ikiwa ni pungufu ya asilimia 16.1 huku gharama nyingine kutokubaliwa hadi hapo watakapopata mtaalamu mshauri atakayefanyia kazi suala hilo na kuona kama viwango hivyo vinafaa.

Alisema kwa marekebisho hayo, bei ya umeme kwa watumiaji wadogo wanaotumia umeme usiozidi kilowati 50 watalipia Sh 60 kwa kila uniti kutoka Sh 49 za awali huku watumiaji wa kawaida watalipia Sh 157 kutoka Sh 129.

Kuhusu kufungua akaunti maalumu, alisema baada ya kukusanya fedha hizo za viwango vipya, Tanesco wanatakiwa kufungua akaunti ya fedha hizo na kuagiza kuwa zielekezwe katika kazi husika ambapo Ewura watakuwa wakikagua kila baada ya miezi mitatu.

Masebu alisema kutokuwakubalia Tanesco kupandisha umeme wasingekuwa na uwezo wa kujiendeleza na vilevile hatua hiyo inatoa nafasi kwa wawekezaji wengine kujiingiza katika sekta hiyo.