.

.

.

.

Wednesday, September 08, 2010

PERFECT KAGISA AFARIKI DUNIA


Maimartha wa Jesse picha kubwa mchumba wa Marehemu Perfect Kagisa juu.

Perfect Kagisa (P.Diddy) amefariki dunia mara baada ya kuanguka ghafla maeneo ya Lumumba alikokuwa ameenda kwa shughuli zake. Rafiki yake wa karibu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bendi ya Diamond Musica Juddy Mosha amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema hivi sasa ndiyo tumetoka katika hospitali ya taifa ya Muhimbili na tayari tumeshahifadhi mwili wa marehemu. Amesema taarifa zaidi zitatolewa na ndugu zake na sasa ndiyo wanaelekea Nyumbani kwao kinondoni kwa ajili ya mipango mingine.
Asha Baraka Mkurugenzi wa Aset naye amesema amepigiwa simu na watu waliokuwepo katika tukio hilo na alichokifanya ni kuhakikisha anampata Mchumba wa Marehemu Maimartha wa Jesse ambaye wakati wa tukio hilo alikuwa kazini kwake TBC anakofanya kazi. Zidi kungalia blogu hii kwa taarifa zaidi juu ya mipango ya mazishi

1 comment:

  1. nampa pole saana maimartha kwa kuondokewa na mtu aliyekuwanae kwenye uhusiano kwa muda mrefu.Najua ni kipindi kigumu sana lakini naomba Mungu ampe faraja na akumbuke wote njia yetu ni moja.

    ReplyDelete