.

.

.

.

Saturday, September 03, 2011

USIKU WA MAVAZI WA REDDS KARIMJEE HALL


Haya ni moja ya mavazi yaliowahi kuvaliwa na wasichana warembo katika miaka ya 1960, mavazi haya ni miongoni mwa mavazi yaliyotia fora katika onyesho la mavazi la Redds Night of Fashion linalofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, lengo la onyesho hilo ni kuwapa ubunifu na kuzindua vipaji mbalimbali vya warembo hao katika jumba la Vodacom House ili kuibua vipaji vyao vilivyojificha. Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ndiyo wadhamini wakuu wa mashindano ya Miss Tanzania kwa muda mrefu sasa.
Mmoja wa warembo akipita jukwaani na vazi lililowahi kuvaliwa katika miaka ya 1960 na wasichana warembo wa miaka hiyo.
Warembo wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania wakicheza ngoma ya Lizombe katika onyesho la Redds Night of Fashion katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
Ankal kulia akiwa katika picha ya pamoja na mchekeshaji Evance Bukuku.
Warembo wakipita na vazi la utambulisho jukwaani kama wanavyoonekana.
Wadau mbalimbali wa urembo wakifurahia jambo katika onyesho la mavazi la Redds Night Of Fashion.
Mdau huyu naye alikukwepo kama unavyomuona akiwa amekula pozi matata.Warembo hawa wakionyesha mbwembwe za kupiga picha jukwaani.
Mpondela akiwa na Meneja wa kinywaji cha Redds Victoria Kimaro wakijadili jambo.
Mapacha watatu katika mambo ya Libeneke kutoka kulia ni Othman wa Mtaa kwa Mtaa, Issa Michuzi wa Michuziblog na Ahmed Michuzi mzee wa jiachie.
Mwanamuziki Banana Zorro akikamua na kundi lake katika onyesho hilo.
Meneja wa Mwasiliano na habari za Mtandao Vodacom Tanzania Matina Nkurlu katikati akiwa na vimwana, waliowahi kufanya vyema katika mashindano ya Vodacom Miss Tanzania mwaka jana kulia ni Salma Mwakalukwa na kushoto ni Consolata Lukosi.
Mdau Shamim Zeze wa 8020 Fashion Blog akila pozi na mrembo Leyla kutoka Redds.
Mkurugenzi wa Benchmark Production Mamaa Ritah Paulsen akila pozi kwa picha na kivazi chake cha kitenge na Chuichui.

Meneja wa uhusiano wa TBL Edith Mushi


KWA HISANI YA FULLSHANGWE

No comments:

Post a Comment