.

.

.

.

Wednesday, April 18, 2012

TSHS. MIL 70 ZATUMIKA KUMZIKA KANUMBA

KAMATI ya mazishi ya aliyekuwa msanii maarufu nchini, Steven Kanumba, imesema imetumia Sh milioni 70 kugharimia maziko yaliyofanyika Aprili 10. 

Kanumba alifariki dunia usiku wa kuamkia Aprili 7 na kuzikwa siku tatu baadaye kwenye makaburi ya Kinondoni na maelfu ya wananchi wa Dar es Salaam na mikoa jirani. 

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mtitu Gabriel alisema jana kwamba kamati hiyo iliyoratibu mazishi ya msanii huyo tangu Aprili 7, ilikusanya michango na ahadi za takribani Sh milioni 90 huku gharama za mazishi hadi maziko vikigharimu Sh 70,502,000. 

Akitoa mchanganuo huo, Mtitu alisema Kamati yake ilitumia Sh 52,102,000 na ahadi za malipo ya vifaa ambazo ni Sh 18,400,000 na zilitumika kwa vifaa mbalimbali zikiwamo taa, jukwaa, viti na maturubai. 

Alisema Sh milioni nne zilizobaki kutokana na zilizokusanywa zilikabidhiwa kwa mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa na Kamati haijatimiziwa ahadi ya Sh milioni 15.5. 

No comments:

Post a Comment