.

.

.

.

Tuesday, September 25, 2012

SERENGETI FREIGHTS YAKABIDHI MSAADA TOKA UK


Mkurugenzi wa kampuni ya usafirishaji mizigi nchini uingereza Serengeti,Bw Chris Lukosi akikabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadiq
Mkuu wa mkoa wa Dar Meck Sadiq akimshukuru Mkurugenzi wa kampuni ya usafirishaji mizigi nchini uingereza Serengeti,Bw Chris Lukosi
Salaam.
Kama tulivyoahidi, leo tumeukabidhi mzigo wa msaada kutoka kwa watanzania waishio UK kwa ajili ya kuwachangia wahanga wa mafuriko yaliyotokea jijini Dar.Mizigo hii imekabidhiwa kwa mkuu wa mkoa wa dar es salaam mheshimiwa Mecky SadiqMzigo huu tumeusafirisha bure na pia tumeulipia ushuru kama mchango wetu kwa wenzetu waliopatwa na janga hili.
Mkuu wa mkoa , kwa niaba ya wanachi wa mabwepande ametoa shukurani kwa  wale wote waliochangia na akatoa mwito kwa wengine kuiga mfano huu wa kutoa.
Sisi Serengeti Freight tunapenda kuwashukuru wale wote waliochangia harambee hii
Pia Tunapenda kutoa shukurani kubwa kwa Jestina George na Urban pulse kwa kushirikiana nasi kukamilisha zoezi hili
KUTOA NI MOYO WALA SI UTAJIRI
Asanteni sana
CHRIS LUKOSI

No comments:

Post a Comment