.

.

.

.

Sunday, July 28, 2013

WAZIRI MWEUSI ITALY ATUPIWA NDIZI




CECIL KYENGE


Italia bado imendelea kukumbwa na wimbi kubwa la ubaguzi wa rangi pale Waziri wa Kwanza Mweusi alipotupiwa ndizi alipokuwa akihutubia katika mkutano wa Chama.
 
Waziri wa Ushirikiano ni Mwitalia wa kwanza mweusi aliyeteuliwa hivi karibuni na amekuwa akipata taabu sana kutokana na dhana ya ubaguzi iliyojengeka miongoni mwa raia wa Italia. Cesile Kyenge ni mzaliwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaye amekuwa akipigania haki ya wahamiaji kupata uraia wa kudumu wa Italia.
 
Muda mfupi kabla ya tukio hilo siku ya Ijumaa, wanachama wa mrengo wa kulia Forza Nuova waliandamana wakipinga kampeni ya Waziri Kyenge ya kutaka kumpa uraia mtu yeyote isipokuwa aliyezaliwa katika ardhi ya Italia.
 
“Uhamiaji Unaua” viliandikwa baadhi ya vipeperushi ambapo ndiyo ilikuwa kauli mbiu ya Forza Nuova wakimaanisha kuwa mauaji mengi yaliyofanyika Italia yalisababishwa na Wahamiaji.
 
Ingawa ndizi alizokuwa akitupiwa zilimkosa, Waziri Kyenge alijibu katika mtanda wa kijamii wa twiter “sad” huzuni kwa kutupa chakula hasa katika wakati huu wa mgogoro wa kiuchumi.
 
“Ujasiri wa kubadilisha hali ya mambo unatoka ndani mwa mtu” alisema waziri Kyenge.
 
Hata hivyo, Waziri Kyenge amekuwa akikabiliwa na matusi mara kwa mara hata kutoka kwa wanasiasa wengine. Mapema mwezi huu, Mbunge mwanamizi wa kaskazini anayepinga sheria ya uhamiaji alimtukana matusi na kumlinganisha na “orangutan” Hata hivyo aliomba msamaha baadaye.
 
 
Sababu ya kumtupia NDIZI ni kuwa imewaudhi FAR-RIGHT PARTY kwa kupendelea IMMIGRATION

No comments:

Post a Comment