.

.

.

.

Friday, October 03, 2008

WAUWAWA KWA AJILI YA SOKO LA TANZANIA

BURUNDI imekumbwa na wimbi la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, albino, kutokana na imani za kishirikina.
Kwa mujibu wa Polisi nchini Burundi hivi sasa maalbino wamelazimika kukimbilia katika hifadhi ya jeshi hilo baada ya kundi la watu kuua maalbino watatu na kuondoka na miguu yao.
Katika albino walionusurika, wanne wamelazimika kujisalimisha katika kituo cha polisi cha Ruyigi na polisi sasa wanatoa ulinzi mkali kwa watu hao.
Tanzania imekumbwa na wimbi la mauaji ya albino na hadi sasa albino 26 wameshauawa katika kipindi cha mwaka mmoja kutokana na imani za kishirikina. Mauaji hayo yansababishwa na imani kwamba viungo vya albino husaidia bahati uchimbaji wa madini na kuwafanya watu watajirike.

No comments:

Post a Comment