.

.

.

.

Saturday, October 29, 2011

YANGA YAIFUNGA SIMBA GOLI 1 KWA O


Mchezaji wa timu ya Yanga Haroub Canavaro akijaribu kumzuia mshanbuliaji wa Simba Felix Sunzu katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom, uliochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.



Kikosi cha timu ya Yanga kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo katika uwanja wa Taifa.
Kikosi cha timu ya Simba kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo kwenye uwanja wa Taifa.
Costadic Papic Kocha wa Yanga ambaye amechukua mikoba ya Sam Timbe ambaye kibarua chake kimeota nyasi kuitumikia klabu hiyo akiwa katika benchi la ufundi la timu hiyo.


Mchezaji wa Yanga Davis Mwape leo amefanikiwa kuwafurahisha mashabiki wa klabu hiyo baada ya kuifungia timu yake goli 1-0 dhidi ya Simba mahasimu wao wakubwa katika kipindi cha pili cha mchezo wa timu hizo Goli hilo pekee lililowafanya mashabiki wa Yanga kulipuka kwa vifijo na nderemo pamoja na kwamba walikuwa ni wachache kuliko wale wa Simba, wakati wakishagilia goli lao huku wakiwaacha wenzao wa Klabu ya Simba wakiwa wameinamia vichwa chini bila kujua la kufanya. Goli hilo pekee la Yanga limewafanya mashabiki wa Simba kuondoka uwanjani huku mpira ukiwa bado haujaisha jambo linaloonyesha jinsi walivyumizwa na goli hilo, wachezaji wa Simba wamekosa magoli mengi na walikuwa na uwezo wa kushinda mchezo huo lakini kitendo cha wachezaji wa timu hiyo kutokuwa makini golini kimewagharimu vya kutosha

No comments:

Post a Comment