.

.

.

.

Wednesday, November 02, 2011

GODBLESS LEMA ................

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema),Godbless Lema

Peter Saramba na Mussa Juma, Arusha
MBUNGE wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ambaye yuko mahabusu, amewataka wafuasi wa chama hicho kumtembelea gerezani kwa wingi leo ambayo ni siku ya kawaida ya kuona mahabusu, akiwataka wasiwe na hofu yoyote kufanya hivyo.

Lema alituma ujumbe maalumu kwa wanachama wa chama hicho akiwataka kuwa watulivu na kumwunga mkono katika harakati zake alizoziita za kupigania haki, usawa na demokrasia ya kweli nchini bila kujali vitisho vya dola.

Katika ujumbe wake huo uliotolewa na Mwenyekiti wa Mfuko wa Maendeleo Arusha (ARDF), Elifuraha Mtowe aliyemtembelea gerezani jana, Lema alisema ameamua kuchukua dhamana ya kukubali kwenda magereza ili kufikisha ujumbe kwa dola na wote wenye kujaribu kuwatisha wenye nia na kiu ya kupigania haki na usawa na kwamba yuko tayari kulipia gharama yoyote kukamilisha ndoto yake.

Aliwataka wananchi kuchanga fedha kwa ajili ya watu aliowakuta Magereza wakitumikia vifungo baada kushindwa kulipa faini walizohukumiwa kwa kutiwa hatiani kwa makosa madogo na alisema tayari ameomba kwa uongozi wa Magereza, orodha ya waliofungwa walioshindwa kulipa faini.

Kwa mujibu wa Mtowe, Lema amewakaribisha wananchi kumtembelea gerezani katika utaratibu wa kawaida wa wafungwa na mahabusu kutembelewa siku za Jumatano, Jumamosi na Jumapili.

Alisema uongozi wa Chadema Mkoa wa Arusha utaratibu ziara hizo kuhakikisha sheria, taratibu na kanuni za Magereza zinazingatiwa kwa wenye nia hiyo.

CHANZO : MWANANCHI

1 comment:

  1. Mkuu utatoka sisi tulionje ya nchi tunaomba Mungu hatutumii akili zetu na hivyo we utatoka tu,acha porisi na serikali yao ya ajabu wafanye vituko,lakini siku ya siku chadema itachukua uongozi.Wananchi tumechoka na ubabe wa serikali isiyojali watu wake.Sisi tunaomba Mungu acha wao watumie akili zao.Mungu akutioe hekima na nguvu.

    ReplyDelete