.

.

.

.

Wednesday, April 25, 2012

WABUNGE KUKWAMISHA BAJETI


KITENDO cha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kushindwa kuzungumzia shinikizo la baadhi ya wabunge kutaka mawaziri wanane wajiuzulu, kimeonekana kuwakera wawakilishi hao ambao sasa wameamua kuibana Serikali huku wakiapa kukwamisha bajeti za mawaziri hao katika Bunge lijalo la Bajeti.
Jana walianza kuonyesha makali baada ya kukataa mapendekezo ya Mfumo wa Mpango wa Mabadiliko wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2012/2013 wakisema hauna jipya na umetayarishwa kwa mfumo uleule kwa miaka 15 mfululizo.

Juzi, Pinda aliahirisha Bunge bila kugusia shinikizo la wabunge hao kutaka Serikali iwawajibishe Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo; Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja; Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu; Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe; Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), George Mkuchika.
Wakizungumza na kwa nyakati tofauti jana, wabunge hao, wengi wao wakiwa ni wa CCM, walisema silaha pekee waliyobaki nayo ni kukwamisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2012/2013 katika kikao kijacho cha Bunge.
Wabunge hao pia wameonya kwamba kutojiuzulu kwa mawaziri hao kutaiweka CCM njia panda katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwani hoja ya ufisadi ndiyo iliyowafanya wenzao wengi wasirudi bungeni.
“Silaha kubwa tuliyobaki nayo sasa ni kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu na nakuambia kama ile karatasi ingerudi upya leo idadi ya wabunge wa CCM ambao wangetia saini ingetikisa nchi,” alisema James Lembeli wa Kahama (CCM)

No comments:

Post a Comment