.

.

.

.

Tuesday, December 04, 2012

JOE KUSAGA AANDAA HAFLA YA CHAKULA CHA USIKU "ESCAPE 2 "


Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akiwakaribisha wageni wake,akiwemo mwanamuziki nyota wa dansi ndani ya kundi la Wenge BCBG,kutoka nchini DRC-Congo,JB Mpiana (pichani kati) kwenye hafla fupi ya chakula cha usiku iliyofanyika kwenye kiota cha maraha cha Escape 2,kilichopo Kunduchi jijini Dar,hafla hiyo pia ni sehemu ya muendelezo wa shamra shamra za maadhimisho ya miaka 13 ya Clouds FM tangu kuanzishwa kwake hapa nchini.
 Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akiwakaribisha wageni wake na kuzungumza nao machache na kuhakikisha wanapatiwa chochote kitu.
 Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimtambulisha mke wake Johayna Kusaga  (ambaye ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Prime Time Promotions Ltd) kwa Mwanamuzik JB Mpiana na kwa wageni wengine waliofika kwenye hafla hiyo ya chakula cha pamoja.
 Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimkaribisha mgeni wake JB Mpiana kwenye chakula
 Pichani ni baadhi ya Washiriki wa shindano la Miss East Afrika  2012 ambao pia waliakwa kwenye chakula cha pamoja ndani ya kiota cha maraha cha Escape 2,kilichopo Kunduchi jijini dar.
 Washiriki wa shindano la Miss East Afrika wakiwa katika picha ya pamoja
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Cassim akitumbuiza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali 
 Boniventure Kilosa a.k.a Dj Venture alikamata mashine na kuangusha ngoma kali zikiwemo za Kinaija,abazo wageni wengi walionekana kuburudishwa nazo vilivyo.
 Washiriki wa shindano la Miss East Afrika 2012 wakijiachia vilivyo kwa mikato ya ngoma iliokuwa ikiangushwa na Dj Venture.
 Joseph Kusaga a.k.a Boss JOe akizungumza na baadhi ya wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Ay na Mwana FA ndani ya hafla fupi ya chakula cha usiku kulichoandaliwa kwa ajili ya wageni.
 Wadau nao walikuwepo.Mdau wa MJ FM pamoja na Andrew Kusaga wakishoo love.
Wafanyakazi mbalimbali kutoka Clouds Media Group walikuwepo pia
Kuserebuka kama hivi pia kulikuwepo
.
 Mtangazaji wa Clouds TV,Ben Kinyaiya akifanya mahojiano mafupi na mwanamuziki mkongwe wa dansi,Ndandaa Kossovo.
 Dj Venture na mshkaji wake wakivuta pumzi.
 Mmoja wa Wakurugenzi wa Prime Time promotios,pichani kulia Godfrey Kusaga akibadilishana mawazo na Mtangazaji mahiri wa kipindi cha Jahazi cha Clouds FM,Ephrahim Kibonde huku wakiangusha moja moja.
 Mazungumzo ya hapa na pale pia yalikuwepo.


Kwa Hisani ya JOHN BUKUKU

No comments:

Post a Comment