.

.

.

.

Friday, January 15, 2010

TAARABU ..........

Mnenguaji hatari toka Kenya Fifi Moto
Maimartha wa Jesse akiongea na wanahabari jijini Dar es salaam jana wakati alipotangaza onyesho kabambe la miondoko ya Taarab linalotarajiwa kufanyika januari 24 kwenye ukumbi wa Traveltine ambalo litajulikana kama Paty Kali la Kufungua mwaka 2010.
Maimartha amesema onyesho hilo litawahusisha wakali wa muziki wa taarab Afrika Mashariki ambo ni Jahazi Molden Taarab, malkia wa mipashi nchini Khadija Kopa na mkali wa kunengua kutoka Nairobi nchini Kenya Fifii Moto ambaye tayari yuko jijini kwa maadalizi kadhaa ya mtikisiko huo wa miondoko ya Taarab.
Maimartha ambaye ni afisa uhusiano wa onyesho hilo amewakaribisha wapenzi wa taarab jijini kuwa tayari kwa burudani nzuri itakayoletwa na wanamuziki hao wakali katika muziki huo akiongezea kuwa Fifii Moto amekuja kuwashika wapenzi na mashabiki wa taarab kwa kiuno chake.

No comments:

Post a Comment