.

.

.

.

Friday, May 04, 2012

VURUGU DAR YOUNG AFRICANS



KWA sasa kuna watu ambao wako msituni, wanatumia baadhi ya wanachama wa Yanga na Waandishi wa Habari kuleta vurugu katika klabu ya Yanga, lengo lao kuuangusha uongozi uliopo madarakani.
Watu hao wanajulikana na silaha yao ni fedha- inawapa jeuri ya kutaka kuivuruga Yanga.
Hadi kufikia hapa, Yanga inakosa hata nafasi ya pili katika Ligi Kuu, wao wamechangia kwa kiasi kikubwa. Kujiuzulu kwa Seif Ahmad ‘Magari’ na Abdallah Bin Kleb katika Kamati ya Utendaji, inasemekana pia kumetokana na ushawishi wao.
Nasikitika watu hawa ni wageni sana Yanga na hawaijui historia ya klabu hiyo. Wana Yanga ni wazito kuamua, kwa sababu wana subira, ila yakiwafika kooni huwa ni wati tofauti sana.
Huwa hawaangalii sura wala hadhi ya mtu.
Mungu amrehemu, Abbas Gulamali, alimwaga fedha nyingi Yanga na akakarabati hadi jengo, kwa ujumla alifanya makubwa nay a kihistoria- lakini alipotofautiana kimisimamo na wenye Yanga yao, yalimgeukia.
Reginald Mengi alikuwa ana heshima kubwa Yanga na akajitolea kusuluhisha mgogoro wa Yanga Asili na Yanga Kampuni.
Awali, walimsikiliza na kwenda naye sawa, lakini alipotofautiana na wenye Yanga yao, yalimgeukia pale Star Light Cinema na hadi leo hajakanyaga tena kwenye shughuli ya Yanga.
Nani asiyejua Mengi ni Yanga mzuri na milionea ambaye leo hii akiangukiwa klabu itakuwa baab kubwa? Tunakubali udhaifu wa uongozi ndani ya klabu, lakini suluhisho lake si kuleta vurugu klabuni.
Kama watu wana vita binafsi, wapambane wao kwa wao bila kuiumiza Yanga. Lloyd Nchunga ni mwana Yanga mmoja tu kati ya mamilioni. Haiwezekani mtu apambane na Mwenyekiti wa Yanga kwa kuinyima Yanga ubingwa- hata nafasi ya pili na bado anataka timu ifungwe na Simba. Huyu si mwana Yanga- ni mnafiki. Ni mbinafsi- na maana yake anataka hata kuwapo Yanga kwa maslahi yake binfasi.
Yanga wa kisasa wanataka umoja, mshikamano na mafanikio ya uwanjani. Yanga wa kupewa noti nyekundu walete malumbano na migogoro isiyo na tija klabuni, hao ni wa kuwaangalia mara  mbili.  
Wewe una umgovi na Nchunga au Yanga, hebu jiulize? Kwa nini uwanyime raha wana Yanga mamilioni kwa mamilioni kwa fedha zako? 

No comments:

Post a Comment