.

.

.

.

Friday, January 04, 2013

SAJUKI APUMUZISHWA KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE

Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Msanii wa Filamu nchini Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) likiwekwa karibu na kaburi tayari kwaajili ya mazishi jijini Dar es Salaam leo.
Rais Kikwete akiweka mchanga kwenye kaburi la Msanii wa Filamu Sadick Juma Kilowoko wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wasanii wakiwa na watu mbalimbali waliohudhuria mazishi ya Msanii Sadick Juma Kilowoko kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Kikwete akijadiliana jambo na Rais wa Shirikisho la Wasanii wa Filamu nchini Simon Mwakifwamba mara baada ya mazishi kwenye makaburu ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo, kushoto ni baba mzazi wa marehemu Mze Juma Kilowoko.
Rais Kikwete akishuhudia safari ya mwisho ya Msanii wa Filamu nchini Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika Kisutu jijini Dar es Salaam.
Baba Mzazi wa Marehemu Sadick Juma Kilowoko (kushoto) akizungumza na Rais Kikwete mara baada ya Mazishi kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo, katikati ni Rais wa Shirikisho la Wasanii wa Filamu nchini Simon Mwakifwamba.
Waandishi wa habari wakichukua matukio mbalimbali wakati wa maziko ya Msanii huyo.
Baadhi ya watu mbalimbali waliohudhuria kwenye msiba huo .
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe akihojiwa na waandishi wa habari kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam muda mfupi kabla ya mazishi ya msanii Sadick Juma Kilowoko.
Rais Kikwete akiwasili kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo kwenye safari ya mwisho ya msanii wa Filamu nchini Sadick Juma Kilowoko (Sajuki).
Jeneza la mwili wa marehemu Sadick Juma Kilowoko, ukienda kupakizwa kwenye gari.
Wakisoma dua baada muda mfupi kabla ya kuondoka nyumbani kwake

No comments:

Post a Comment