.

.

.

.

Monday, October 07, 2013

AL-SHABAB WASHAMBULIWA NCHINI SOMALIA

Wafuasi wa Kundi la Al-Shabaab nchini Somalia wamesema kuwa mji wao Kusini mwa Somalia umeshambuliwa na wanajeshi wa mataifa ya Magharibi.
Wapiganaji hao walisema wanajeshi wa kigeni waliuvamia Mji wa Barawe usiku wa manane.
Baadhi ya taarifa zinaeleza kuwa helikopta ilitumiwa kwenye shambulio hilo.
Wengine wanaeleza kuwa wanajeshi waliingia usiku wakitokea maeneo ya pwani.
Al-Shabab ilisema shambulio hilo halikufanikiwa ingawa inakiri mpiganaji wao mmoja aliuawa.
Kundi hilo linadai kuwa wanajeshi maalumu wa Uingereza na Uturuki ndio waliofanya shambulio lakini hayo yalikanushwa na Uingereza na Uturuki.
Jina Al-Shabaab linamaanisha Kijana  kwa lugha ya Kiarabu. Kundi hilo liliibuka kama Tawi la Vijana la Muungano wa Mahakama za Kiislamu ambao baadaye ulivunjika mwaka 2006.
Chanzo cha kuvunjika kwa muungano ni baada ya kundi hilo  lilipopigana na wanajeshi wa Ethiopia waliokuwa wameingia nchini Somalia kuunga mkono Serikali ambayo ilidaiwa kuwa ilikuwa ni  dhaifu.

No comments:

Post a Comment