.

.

.

.

Tuesday, November 25, 2008

BREAKING NEWS: MRAMBA NA YONA KIZIMBANI

Mawaziri wa zamani mh. Daniel Yonah (shoto) na mh. Basil Pesambili Mramba wakiwa katika mahakama ya hakimu mkazi ya kisutu jijini dar baada ya kusomewa mashtaka yao muda mfupi uliopita.
wah. Yona na Mramba wanakabiliwa na jumla ya mashataka 13 ikiwa ni pamoja na kutumia vibaya madaraka yao walipokuwa mawaziri, kuingia mikataba ya madini na kadhalika. stori kamili inaandaliwa.
wote wamewekewa masharti ya dhamana kwamba kila mmoja atoe bilioni 3.9 keshi, wasalimishe hati za kusafiria, wasitoke nje ya dar na kila mmoja awe na wadhamini wawili ambao mahakama inabidi iridhike kuwa ni wa kuaminika.


Taarifa zilizopatikana toka bongo zinasema Wah. hao wamepelekwa keko rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana .Kesi hiyo imepangwa kutjwa tena mahakamani hapo tarehe 5 desemba 2008.

No comments:

Post a Comment