.

.

.

.

Wednesday, January 19, 2011

KAPUMZIKE KWA AMANI JAJI MSTAAFU MAPIGANO



Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi akisoma kwa huzuni kipeperushi kinachoelezea wasifu wa marehemu Jaji mstaafu, Dan Mapigano wakati wa shughuli ya kutoa heshima za mwisho, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)


Mjane wa marehemu Jaji mstaafu, Dan Mapigano, Florence (wa pili kulia) na mwanawe, Shila Mapigano (wa pili kushoto) wakiwa na Spika wa zamani wa Bunge la Afrika, Getrude Mongela (kushoto) pamoja na Mke wa Spika wa zamani wa Bunge la Tanzania, Samuel Sitta, Maragareth Sitta, wakati wa shughuli ya kutoa heshima za mwisho, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

Jaji Kiongozi, Fakhi Jundu

Baadhi ya waombolezaji


Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba akiwasili kutoa heshima za mwisho
Jaji mstaafu, Robert Mihayo akisoma wasifu wa Marehemu Mapigano

Ali Hassan Mwinyi akimfariji mtoto wa Jaji Mapigano, Shila.


Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, akitoa heshima za mwisho kwa Marehemu Jaji Dan Petro Mapigano nyumbani kwake Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Marehemu Dan amezikwa leo jijini Dar es Salaam.

PIcha kwa Hisani ya RICHARD MWAIKENDA

1 comment:

  1. Mungu akulaze mahala pema peponi Jaji Mapigani... Nitakukumbuka kwa utu wako uliotukuta!

    ReplyDelete